USHAIRI MASWALI NA MAJIBU
Joseph Kiponda : Taifa ni UshuruLau kama ingakuwa, madhali tuna uhuru Watu kodi kutotowa, na kuifanya kufuru Vije nchi ingakuwa, taifa bila ndururu Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Hivi taifa kumea, nakuendelea mbele Kwamba lajitegemea, haliwategei wale Yataka kujitolea, ushuru bila kelele Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Wafanyikazi wa umma, mfano mwema walimu Wauguzi mahashuma, daktari wahadimu Bila hizi darahima, vipi wangalihudumu? Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Si vyema kuombaomba, kwa wageni kila mara Huwa twajifunga kamba, na kujitia izara Adha zinapotukumba, kujitegemea bora Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru. Miradi ya maendeleo, yahitaji darahima Ndo tufikie upeo, ulio dunia nzima Wadogo na wenye vyeo, bila kodi tutakwama Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Ushuru si kwa wanyonge, wasokuwa na uwezo Watozwe hata wabunge, na wengine wenye nazo Yeyote asijitenge, kodi akalipa bezo Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Kwetu kutoa ushuru, ndiko kujitegemea Pasiwepo na udhuru, sio wa kuelea Huwa ni kama kiguru, asenao kutembea Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru. Maswali
MAJIBU
0 Comments
|
AuthorAtika School Team Archives
June 2024
Categories
All
|
We Would Love to Have You Visit Soon! |
Hours24 HR Service
|
Telephone0728 450425
|
|
8-4-4 materialsLevels
Subjects
|
cbc materialsE.C.D.E
Lower Primary
Upper Primary
Lower Secondary
Upper Secondary
|
teacher support
Other Blogs
|