USHAIRI MASWALI NA MAJIBU
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswaliDaima alfajiri na mapema Hunipitia na jembe na kotama Katika njia iendayo kondeni Kama walivyofanya babuze zamani; Nimuonapo huwa anatabasamu Kama mtu aliye na kubwa hamu Kushika mpini na kutokwa jasho Ili kujikimu kupata malisho. Anapotembea anasikiliza Videge vya anga vinavyotumbuiza Utadhani huwa vimemngojea Kwa usiku kucha kuja kumwimbia; Pia pepo baridi kumpepea Rihi ya maua zikimletea Nao umande kumbusu miguu; Ni miti yote hujipinda migongo Kumpapasa, kumtoa matongo; Na yeye kuendelea kwa furaha Kuliko yeyote ninayemjua Akichekelea ha ha ha ha ha ha ha … Na mimi kubaki kujiuliza Kuna siri gani inayomliwaza? Au ni kujua au kutojua? Furaha ya mtu ni furaha gani Katika dunia inayomhini? Ukali wa jua wamnyima zao Soko la dunia lamkaba koo; Dini za kudhani zamsonga roho Ayalimia matumbo ya waroho; Kuna jambo gani linamridhisha? Kama si kujua ni kutokujua Laiti angalijua, laiti angalijua! Maswali
majibu ya ushairi
(a) – Ukali wa jua unaharibu zao. - Soko la dunia ni mbaya. - Dini za kudhani zamsonga roho. - Analimia waroho au wenye pupa. (4x1) (b) Tashbihi – Katika njia iendayo kondeni - Kama walivyofanya babuze zamani. Balagha - Kuna jambo gani linamridhisha -Kuna siri inayomliwaza. Tanakali za sauti – Alichekelea ha ha ha ha … Taswira - videge vya anga vinavyotumbuiza Tashihisi – Nao umande kumbusu miguu. Msemo - kumkaba koo – kuumiza. Takriri - Laiti angalijua, laity angalijua. (4x2) (c) Mkulima (1x1) (d) Malalamishi/huruma (1x1) (e) Kuboronga sarufi - Kama mtu aliye na hamu kubwa. - Lahaja - kotama. (2x1) (f) Kila asubuhi anapita akiwa na jembe akielekea shambani. Kama walivyofanya babu zake.Ninapomuona huwa ana furaha kama mtu aliye na tamaa kubwa ya kulima na kutokwa na jasho ili apate kujilisha. (4x1)
0 Comments
Joseph Kiponda : Taifa ni UshuruLau kama ingakuwa, madhali tuna uhuru Watu kodi kutotowa, na kuifanya kufuru Vije nchi ingakuwa, taifa bila ndururu Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Hivi taifa kumea, nakuendelea mbele Kwamba lajitegemea, haliwategei wale Yataka kujitolea, ushuru bila kelele Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Wafanyikazi wa umma, mfano mwema walimu Wauguzi mahashuma, daktari wahadimu Bila hizi darahima, vipi wangalihudumu? Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Si vyema kuombaomba, kwa wageni kila mara Huwa twajifunga kamba, na kujitia izara Adha zinapotukumba, kujitegemea bora Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru. Miradi ya maendeleo, yahitaji darahima Ndo tufikie upeo, ulio dunia nzima Wadogo na wenye vyeo, bila kodi tutakwama Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Ushuru si kwa wanyonge, wasokuwa na uwezo Watozwe hata wabunge, na wengine wenye nazo Yeyote asijitenge, kodi akalipa bezo Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru Kwetu kutoa ushuru, ndiko kujitegemea Pasiwepo na udhuru, sio wa kuelea Huwa ni kama kiguru, asenao kutembea Taifa halingakuwa, bilashi bila ushuru. Maswali
MAJIBU
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.Maendeleo ya umma Sio vitu maghalani Kama tele vimesaki Lakini havishikiki Ama havikamatiki Bei juu Maendeleo ya umma Sio vitu gulioni Kuviona madukani Kuvishika mikononi Na huku wavitamani Kama tama ya fisi Kuvipata ng’o Maendeleo ya umma Sio vitu shubakani Dhiki ni kwa mafakiri Nafuu kwa mafakiri Ni wao tu washitiri Huo ni uistimari Lo! Warudia Maendeleo ya umma Ni vitu kumilikiwa Na wanyonge kupatiwa Kwa bei kuzingatiwa Bila ya kudhulumiwa Na hata kuhadaiwa Hiyo ni haki. Maendeleo ya umma Dola kudhibiti vitu Vijapo nchini mwetu Na kuwauzia watu Toka nguo na sapatu Pasibakishiwe na kitu Huo usawa. Maendeleo ya umma Watu kuwa na kauli Katika zao shughuli Vikaoni kujadili Na mwisho kuyakubali Maamuzi halali Udikteta la. Maendeleo ya umma Watu kuwa waungwana Vijakazi na watwana Nchini kuwa hakuna Wote kuheshimiana Wazee hata vijana. Maswali
majibumajibu
Soma shairi kisha ujibu maswali Nizike Ningali Hai!: Hassam Muchai Kipusa Binti Hamadi, siku n’takuwa kimba Nizikwe Kifudifudi, na yoyo kuyumbayumba Takuwa bure biladi, matozi ungayasomba Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika Tena ningaumwa ungo, na mapumu kuugua Lioze ini na nyongo, na pua zisipumua Takuwa sina kinyongo, mradi nimeshatua Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika Nizike sasa mwenzangu, nizike ningali hai Singojee kufa kwangu, uanze kurairai Kulilia kifo change, ni bure hakukufai Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika Nikifa hutonizika, kimwana sanda nunua Manukato ya kupaka, na nguo za kuanua Nivishe sione shaka, Washindwe kupambanua Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika Tena nikande misuli, nikande pande kwa pande Siate kiwiliwili, shingo, miguu ikande Umalizapo kiwiliwili, mwenzangu niende shonde Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika MASWALI
MAJIBU
maswali 10 ya chaguzi zaidiHapa kuna seti ya maswali 10 ya chaguzi zaidi.
MAJIBU YA MASWALI 10 YA CHAGUZI
Hapa kuna majibu kwa maswali yaliyotolewa:
Soma shairi kisha ujibu maswali Ndugu ona mbwa yule, ambaye ananyekenya; Yaone mabuu yale, ambayo yamchezeya; Kuwa leo yuafile, mwili yanautaniya; Jana awile jasiri! Juzi shujaa awile, pasiwe kumfikiya; Kwenye makani yale, alipojisururiya; Leo kuwa yuafile, mainzi yamchekeya; Jana awile Jasiri! Mijino mikubwa ile, ambayo ‘mejitokeya; Yali kiwaliza wale, karibu walosogeya; Tena akibweka yule, waoga walijinyiga; Jana awile jasiri! Kamwe kuishi milele, kupe ukajinyonyeya; Walo chini yako wale, muhali unawaziya; Ameshindwa yule pale,sembuse wewe sikiya; Jana awile jasiri! Kama walo hai wale, yafaa kuzindukiya; Ni dunia maji male, muhimu kujiwaziya; Wazipunguze kelele, na kwingi kujishauya; Jana awile jasiri! Maswali
Majibumajibu
MASWALI 10 YA CHAGUZIHapa kuna seti ya maswali 10 ya chaguzi zaidi.
MAJIBU YA MASWALI 10 YA CHAGUZI
Hapa kuna majibu kwa maswali yaliyotolewa:
|
AuthorAtika School Team Archives
June 2024
Categories
All
|
We Would Love to Have You Visit Soon! |
Hours24 HR Service
|
Telephone0728 450425
|
|
8-4-4 materialsLevels
Subjects
|
cbc materialsE.C.D.E
Lower Primary
Upper Primary
Lower Secondary
Upper Secondary
|
teacher support
Other Blogs
|