Maswali na Majibu KCSE Kiswahili
Ufahamu | Ufupisho | Isimu Jamii | Insha | Utumizi wa Lugha
Majibu
SWALI LA 1. -Mwanafunzi aandike insha yenye kuhusu mazungumzo au majibizano kati ya wahusika hawa watatu -Insha ifuate mtindo wa mchezo wa kuiguza - Azingatie kisa cha utovu wa nidhamu kama vile kupigana na mwanafunzi mwenzake, kuchelewa, kutovaa sare za shule n.k - Mwanafunzi atumie maneno mia nne (400). Asiyefikia maneno mia nne aondolewe maki 2 yaani 2u - Asipozingatia sura aondilewe maki 4 yaani 4s. SWALI LA 2
Faida ya kuelimisha motto wa kike
Maana ya methali SWALI LA 4 -Mwanafunzi atunge kisa ambacho kitaonyesha kuwa anajuta baada ya kutozingatia mawaidha -aliyopewa hapo awali -Mwanafunzi asiyemalizia kwa maneno haya awekwe katika kiwango cha D (alama3) -Akiongeza au kupunguza maneno matano aondolewe alama 2 yaan 2M
0 Comments
ISIMU JAMII4. ISIMU JAMII (a) Pambanua sifa zozote sita za lugha rasmi (alama 6) …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (b) Ni mambo yapi yanayotambulisha sajili ya vijana? (alama 4) …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... 4. ISIMU JAMII
(a) Sifa za lugha rasmi:
MATUMIZI YA LUGHA3. MATUMIZI YA LUGHA (a) Akifisha kifungu kifuatacho. (alama 3) nilipowasili tu nilishika tama nikashangaa loo moto huo ulianza vipi na ulikuwa umesababishwa na nini nilishikwa na bumbuwazi magoti yangu yakaanza kuchezacheza. …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (b) Tunga sentensi moja katika umoja kisha uigeuze ili iwe katika wingi ili kudhihirisha ngeli ya LI – YA. (alama 2) (i) …………………………………………………………………………………………………… (ii)…………………………………………………………………………………………………… (c) Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia jedwali. (alama 2) Baba anafyeka nyasi ilhali mtoto anaambua viazi …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (d) Andika katika msemo wa taarifa: (alama 4) Zainabu : Aa! Mbona umeketi peke yako kaka? Wenzako wajistarehesha huku na huko, wewe umekaa pweke, kwa nini? Una mkasa gani? Kagame: Sina mkasa wowote, dada, ila nasumbuliwa na ugeni tu. Niliwasili hivi juzi na sijapata sahibu hata mmoja, ndiyo sababu ukaniona katika hali hii ya upweke …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (e) Sahihisha sentensi zifuatazo bila kugeuza maana. (i) Mtume mwenye wamefika ni mrefu. (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Twiga hukimbilia mbio ingawa ni ndefu. (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………… (f) Andika kwa wingi: (alama 2) (i) Uta uu huu ndio aliotumia kumfuma swara. ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Ugomvi wake ulisababisha kutalikiwa kwake ……………………………………………………………………………………………………… (g) Unda nomino mbilimbili kutoka kwa vitenzi: (alama 2) (i) Fuata ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Zika ……………………………………………………………………………………………………… (h) Bainisha maana katika sentensi zifuatazo. (alama 2) (i) Isije ikawa Maria anahusiana naye …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (ii) Huenda ikawa amepitia njia nyingine. …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (i) Andika upya ukitumia – o –ote (alama 2) (i) Kitabu kikipendwa na wasomaji wengi huwa maarufu. ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Kila askari apitaye hapo humchapa. ……………………………………………………………………………………………………… (j) Tunga sentensi moja itakayodokeza matumizi mawili tofauti yas kiambishi ’ka’ (alama 2) …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (k) Badilisha hadi katika hali ya udogo. (alama 2) (i) Uta.......................................................................................................................................... (ii) Kijiko....................................................................................................................................... (l) Toa maana mbilimbili kwa kila moja ya maneno haya: (alama 2) (i) Kata …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (ii) Ua …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (m) Andika sentensi ifuatayo katika umoja. (alama 2) Nyua zenu zanuka kwa sababu hamzitumii kwa uangalifu. ……………………………………………………………………………………………………… (n) Tunga sentensi moja sahihi ukitumia kivumishi kimilikishi. (alama 2) ……………………………………………………………………………………………………… (o) Bainisha wakati na hali katika sentensi: (alama 2) Utakapofika nitakuwa nimekula. …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………........ (p) Iandike upya sentensi ifuatayo ukifuata agizo. (alama 2) Hakika Mogeni alimcharaza mno Manoti, lakini sidhani kuwa kichapo pekee kingepelekea aliyetwangwa kulazwa hospitalini: (Anza: Sidhani...........................) …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (q) Eleza maana za: (alama 1) (i) Kuteka nyara ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Kujenga nyumba za karata (alama 1) …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (r) Taja methali moja inayofungamana na maelezo yafuatayo: (alama 1) Wakati mwingine mtu hujikuta au hupatikana asipotarajiwa, asipokusudia ilhali hana makosa au hitilafu yoyote. ……………………………………………………………………………………………………… (s) (i) Kanusha: Waimbaji walio maarufu wamepata tuzo. (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………… (ii) Andika kinyume cha sentensi: Mama alimeza dawa yote. (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………… 3. LUGHA (a) Nilipowasili tu nilishika tama. Nikashangaa, “Loo! Moto huo ulianza vipi na ulikuwa umesababishwa na nini?” Nilishikwa na bumbuwazi. Magoti yangu yakaanza kuchezacheza 12 x ¼ = 3 (b) (i) Jitu hilo lilinishtua sana usiku huo. (ii) Majitu hayo yalitushtua sana usiku huo - sentensi zaweza kuwa tofauti 2 x 1 =2 (d) Zainabu alishangaa kumwona Kagame ameketi peke yake amesononeka huku watu wengine wakistarehe. Kagame alimfahamisha kwamba hakuwa na mkasa wowote ila alikuwa anasumbuliwa na ugeni tu; hakuwa amepata rafiki au sahibu Alama 4
(e) (i) Mtume aliyefika ni mrefu Mitume waliofika ni warefu (ii) Twiga hutimka/ hukimbia mbio ingawa ni mrefu 2 x 1 = 2 (f) (i) Nyuta zizi hizi ndizo walizotumia kuwafuma swara (ii) Ugomvi wao ulisababisha kutalikiwa kwao 2 x 1 = 2 (g) (i) Kufuata, mfuasi, mfuatano (ii) Kuzika, maziko, mzikaji, mazishi 4 x ½ = 2 (h) (i) Kuhofia isitokee kuwa hivyo (ii) Kutokuwa na uhakika; kukisia 2 x1 = 2 (i) (i) Kitabu chochote kikipendwa na wasomaji wengi huwa maarufu (ii) Askari yeyote apitaye hapo humchapa 2 x 1 = 2 (j) Alifika nyumbani, akaketi kisha akapiga simu Zozote 2 x 1 = 2 (k) (i) Kijiuta (ii) Kijijiko 2 x 1 = 2 (l) (i) Kata – Eneo la kusimamia watu - Kifaa, hasa cha kuchotea maji - Hali ya kutenganisha k. m. uhusiano (ii) Ua – fisha au toa uhai (kitenzi) - Pambo (wingi maua) (nomino: LI – YA) - Eneo lizungukalo nyumba au boma (wingi nyua – U – ZI) 4 x ½ = 2 (m) Ua wako wanuka kwa sababu huutumii kwa uangalifu 4 x ½ = 2 (n) Changu, letu, mwangu 1 x 2 = 2 (o) Wakati ujao, hali timilifu 2 x 1 = 2 (p) Sidhani kuwa kichapo pekee kingepelekea Manoti kulazwa hospitalini ingawa hakika Mogeni alimcharaza mno Alama 2 (q) (i) Kuvamia au kutia mikononi au kuficha kwa nia fulani (ii) Kuota au kufikiria yasiyowezekana haraka 2 x 1 = 2 (r) Mtego wa panya huingia waliomo na wasiokuwamo 1 x 1 = 1 (s) (i) Waimbaji wasio maarufu hawajapata tuzo (ii) Mama alitema dawa yote UFUPISHO2. UFUPISHO Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali. Ukimwi ni ufupi wa ukosefu wa kinga mwilini. Uwele huu ni wa zinaa ambao hauna tiba, dawa wala kafara. Insi anaweza kupata wiche ya ukimwi kwa njia ainati. Mathalani ni; kujamiiana baina ya mwanamume na mwanamke japo wote au mmoja ana wiche ya virusi vya ukimwi. Nina aliyehimili anaweza kumtia wiche mtotowe akijifungua au kwa kumnyonyesha. Katika harakati na mikakati ya kutoa damu, au ngeu hiyo kuchangamana na jeraha nyevu. Cheche akilia mfiche kuku, ama fisi akimia mwele funga mlango. Tuupige ukimwi vita shadidi, kwani si lelemama. Tutahadharike kabla ya athari kwani hadi sasa hakuna tiba hususan, ya uwele huu. Tarakimu zinabainisha kwa kina kuwa vijana wengi ndio wanaoathirika. Wengi wao wamefufutika na kugugunwa wakabakia mifupa. Hali kama hii ikishitadi kujiradidi nchi hii yetu itakosa viongozi wa mustakabali. Wimbo mui hauongolewi mtoto. Wazazi wanafaa kuwa kielelezo chema kwa wana wao. Mwana akibebwa hutazama kisogo cha ninake. Ni jambo la fedheha na kukereketa mtima kuwaona baadhi ya wazee wakichana mtaani vipara moto. Vijana hutegwa kwa chachu na kunaswa kwa ulimbo. Pengine huingia mitegoni kwa ghiliba chache tu za pesa nane. Enyi vijana jihadharini! Wazee hawa ni vitaange watawatosa demani. Mila na tamaduni nyingine zimepitwa na wakati. Wala hazina nafasi katika dunia ya sasa. Tunafaa kutembea na wakati kwani tusipoukata utatukata. Swala la kuingia mafa wajane wafaruku limekita mizizi miongoni mwa makabila humu nchini. Hili ni swala nyeti linalohitaji kuvuliwa nguo livaliwe nduruga. Serikali sharti iingilie kati na kukata kauli kuukomesha uozo na uvundo wa namna hii. Ukata na uchochole umechangia pakubwa katika kuupalilia mbolea ukimwi. Kwa sababu ya uchechefu wa fulusi za karo, shababi wengi hawamudu kuendelea na masomo. Kitembo cha elimu hakikiuki elimu ya msingi. Zaidi, mwanamume wa kisasa ambaye bado amefungwa pingu na taasubi za kiume hapendezwi na hali hii na huuma kidole akitamani ya kale. Shingo upande analazimika kukubali kuwa mabadiliko ni jambo la aushi. Mla kunde hunya kunde. Vijana lazima watahadharishwe na malimwengu. Wasije kufa na laiti ningalijua, na chanda kili kinywani. Wengi wamezizika mila na tamaduni katika kaburi la sahau. Hawaoni hawasikii kwa sababu hawana ashiki. Wameuvua utu wakajivika uchu. Matongozi yamejaa tadabui tena, masikio yamejaa komango yasiweze kusikia. Ukimwi unawagegeda na kuwakeketa kama umwa. Utamu unapoisha wanatemwa na kutiwa mavani kama makapi. Wanafaa kuaswa waasike kwa maaso yenye adili. Ulimwengu kokwa ya fuu haiishi utamu, anayeisha ni binadamu. Maswali (a) Fupisha ujumbe unaojitokeza katika aya tano za kwanza za makala haya. [Maneno 50 – 60] [Alama 8,2 za utiririko] Matayarisho …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... Jibu …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... (b) Katika aya za sita na saba, mwandishi anawashauri waja. Toa nasaha hiyo. (Maneno 35 – 45 ) (Alama 7, 1 ya utiririko) Matayarisho …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... ……………………………………………………………………………………………………… Jibu …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... …………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………......... 2. UFUPISHO
(a) UKIMWI – Ugonjwa wa zinaa usiokuwa na tiba Mama anaweza kumwambukiza mtoto, wakati wa kuzaa au kunyonyesha Damu ikichanganyika baina ya watu ni hatari Watu waepukane na UKIMWI kwa vile ni hatari Vijana waonywa dhidi ya wazee waasherati Mila zingine zimepitwa na wakati Serikali ina sera mbovu kuhusu mila Umaskini huchangia UKIMWI Ni wajibu wa serikali kupambana na janga hili Zozote 6 x 1 = 6 (b) Watu kuelimika/kuelimishwa waepukane na maafa Vijana waonywa kuepuka maovu Vijana waenzi mila za jamii zao; wasitupe tamaduni/desturi Watu watii wanayoambiwa na wakuu Kuzingatia maadili Kujiepusha na tamaa nyingi za ulimwengu Kuwa na utu – kutahadhari na UKIMWI Zozote 6 x 1 = 6 UFAHAMu 1. UFAHAMU Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Tukilinganisha maisha ya zamani na ya siku hizi tutaona kwamba mambo mengi sana yamebadilika. Si watu wazima, si watoto; sote tumeathirika si haba. Mitindo mipya ya kimaisha na mazingira yanayobadilika kasi ni baadhi tu ya mageuzi haya. Sio katika mavazi, lugha, mienendo, mitizamo, mawazo na mielekeo tu bali katika vipengele vingi vingine. Mavazi ya zama hizo yalikuwa yakitengenezwa kutokana na maganda ya mti au ngozi za wanyama kama vile mbuzi, kondoo, punda, ngamia, ng’ombe na hata pengine wanyama wa mwituni. Kwa vile kila mtu alifuga wanyama wengi, hakukuwa na shida ya kuzipata ngozi kama hizo wakati wowote ule haja itokeapo. Magome ya miti yalipatikana mwituni – na kwa kuwa katika enzi hizo hakukuwa na hifadhi za wanyama wa mwitu wala miitu yenyewe, watu waliweza kuingia katika pori lolote na kubambua maganda au kuua wanyama kama walivyohitaji. Mavazi yalikuwa rahisi kupatikana kuliko zama zetu; licha kwa upande wa ndarama, hata kwa upande wa sheria pia. Zaidi, katika enzi hizo watu hawakujali kwenda uchi au walipachika kipande tu cha vazi mwilini. Siku hizi gharama ya maisha imepanda mno. Siku hizi hatuwezi kuwaua wanyama wa mwituni vururu mtende eti kwa chakula, kama walivyofanya babu zetu. Enzi hizo matunda yalining’inia mitini na njaa zilikuwa si nyingi. Chakula kilikuwa bwerere zaidi ya leo. Vinywaji vilikuwa kwa mpango – wazee wa ngambi walikuwa na vinywaji vyao; wazee wa kawaida, wanawake na watoto hirimu hawakusahauliwa. Watu waliheshimiana; vijana walikuwa wenye adabu na walifahamu fika kuwa walipaswa kuwaheshimu wakubwa kwa vyovyote vile. Siku hizi vyakula ni haba na ghali na vingi vyazua magonjwa tata. Siku hizi kuna weledi wengi, hasa wa sayansi. Mja akitaka kwenda safarini huchukua kidubwasha fulani na huyoo! Kaenda zake; barabarani, angani au hata katikati ya kilindi cha bahari. Leo twajivunia ujuzi na maendeleo ya kiafya na madawa yapunguzayo mno unyofu wa binadamu lakini bado kuna pengo kubwa kati ya vikongwe na watu wa makamo, kinyume na zama hizo. Maisha ya karne hii yamekuwa kama zile nguo ziitwazo“bwaga – mtwae’’, ambazo hazibali kufumka au kukwajuka. Hivi leo, mtu akiumwa na kichwa hukimbilia kwa daktari. Mwingine akiumwa na nyoka popote pale, hukimbilia hospitalini akapate sindano ambayo hata jina lake halijui. Zamani ilikuwa mtu achimbechimbe mizizi ya upuzi upuzi, aitafune na alipata nafuu! Wa kisasa twawapuuza wa kale eti hawakujua elimu ya usafi tuijuavyo sisi, ilhali walikuwa wakiichoma miili ya watu waliokuwa wamekufa kwa ukoma au kifua kikuu. Wakati mwingine walikihama kijiji kilichoingiliwa na maafa ya ndui. Hata sasa wagonjwa kama hao hutengwa hospitalini huku maradhi kama vile UKIMWI bado yakikosa tiba. Mengi tuliyonayo sasa, mathalan tarakilishi na eropleni yalivumbuliwa au kugunduliwa na hao wa zamani. Fanaka zetu zote na ustawi tulionao asili yake ni watu hao wa zamani. Akili ni mali na kila mtu ana zake. Kuongezeka kwa watu duniani, mchanganyiko au matumizi mabaya ya madawa mengi pamoja na uchafuzi wa hali ya anga pia yameongezea kuleta hasara kubwa. Kweli sikio haliwezi kushinda kichwa. (a) Kulingana na mwandishi, kwa nini maisha ya kale na ya sasa hayalingani? (alama 3) .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... (b) Kupata mavazi zama zile kulikuwa nafuu. Toa sababu. (alama 2) .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... (c) Kwa kusema siku hizo, ’chakula kilikuwa bwerere zaidi ya leo,’ mwandishi anamaanisha nini? (alama 2) .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... (d) Taja sababu za magonjwa na maafa kukithiri siku hizi licha ya hatua kubwa katika elimu na afya. (alama 3) .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... .......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................... (e) Fafanua usemi, ’sikio haliwezi kupita kichwa’ kwa mujibu wa taarifa. (alama 2) (f) Eleza maana ya: (i) Magome – (ii) Vururu mtende – (iii) Hazibali - (alama 3) 1. UFAHAMU
(a) Mabadiliko ya maisha/athari za kigeni/mitindo mipya ya kimaisha;, mavazi, chakula, afya nk. Mazingira yanayobadilika – Sheria zinabadilika Teknolojia, tarakilishi nk. Zozote 3 x 1 = 3 (b) Wanyama walifugwa kwa wingi Misitu ilikuwa kocho Watu walikuwa huru hata kuwinda na kukata miti Zozote 2 x 1 = 2 (c) Chakula kilipatikana kwa urahisi mno na bila malipo au gharama kubwa. 1 x 2 = 2 (d) Idadi kubwa/kuongezeka kwa watu duniani Mazingira yanayobadilika mara kwa mara Mchanganyiko au matumizi ya madawa mengi pamoja Uchafuzi wa hali ya anga Zozote 3 x 1 = 3 (e) Vijana si sawa na wazee; watu wazima wana hekima, busara na tajriba ya maisha Watu wa siku hizi hawawashindi wa zamani kimaisha 2 x 1 = 2 (f) (i) Maganda ya miti (ii) Ovyo ovyo bila woga au vikwazo (iii) Hazikawii; hazichukui muda ; hazihimili 3 x 1 = 3 ISIMU JAMII4. ISIMUJAMII
Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali: A: ohh, dada Naomi B: Dada Ruth (anamsogea kwa bashasha wanakumbatiana). Ahh Mungu asifiwe! A: Asifiwe sana B: Ehh dadangu, miezi…mingi…sijakuona A: Dada wee…nilitumwa huko kusini…kuwahubiria watu injili (mtuomdogo) singeweza kukataa… B: Ehh, usiwe kama yona A: Habari ya siku nyingi? B: Nzuri Mungu bado ameendelea kunibariki A: Amen! B: Nimeendelea kuiona neema yake A: Amen! Asifiwe Bwana B: Halleluya A: Ni Mungu wa miujiza! B : Amen. Hata nami niko imara katika siku hizi za mwisho A: Amen! B: Ni Mungu wa ajabu kweli! A: Nilikumbana na matatizo lakini nikategemea sala Kama Paulo na Sila …Na nikashinda (anatua). Siwezi kumpa shetani nafasi...maana ameshindwa. B: Ameshindwa kabisa. Maswali:- (i) Hii ni sajili ya wapi? Fafanua (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Taja na ueleze sifa za sajili hii .(al.6) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (iii) Taja na ueleze mambo mawili yaliyosaidia katika maenezi ya Kiswahili Afrika mashariki na kati. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… MATUMIZI YA LUGHA3. MATUMIZI YA LUGHA
(a) Jaza mapengo Kutenda Kutendesha (i) Chota …………………… …………………………… (al.1) (ii) Lewa …………………… …………………………… (al.1) (b) Taja sauti moja ya; (i) King’ong’o (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Kiyeyusho (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (c) Tumia neno “shujaa” katika sentensi kama:- (i) Kivumishi (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Kielezi (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (d) Tambua vitenzi katika sentensi hii kuvipigia mistari :- Sisi tulikwisha kutambua alikuwa na nia mbaya. Yeye ndiye mwizi. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (e) Andika wingi wa sentensi hii sentensi hii hali ya ukubwa:- Kichinjio hiki kilikarabatiwa kwa pesa nyingi. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (f) Eleza maana zinazojitokeza katika vifungu vifuatavyo:- (i) Jambazi kutoka dukani liliiba. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Liliiba jambazi kutoka dukani. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (iii) Kutoka dukani jambazi liliiba. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (iv) Jambazi liliiba dukani. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (g) Jaza neno ambalo ni kinyume cha lile lililopigiwa mstari katika sentensi:- (i) Vile vitu ulivyochanganya itakubidi. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Bomba hili limeziba mwite fundi aweze. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (h) Unganisha sentensi hii kwa kutumia ‘o’ rejeshi. Wavu umekatika. Wavu ni wao. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (i) Eleza matumizi mawili ya “ka” na utunge sentensi kwa kila mojawapo. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (j) Yakinisha sentensi hii Sijafahamu kwa nini hawamkaribishi mpwa wao. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (k) Andika katika usemi halisi:- Mama aliwahimiza warudi siku hiyo la sivyo wangekosa tuzo. (al.3) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (l) Akifisha sentensi ifuatayo:- Sijaona kitabu kizuri kama mayai waziri wa maradhi, utaniazima siku ngapi bashiri alimwuliza rita. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (m) Changanua kwa njia ya mishale Mama anapika na baba anasoma gazeti. (al.4) …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (n) Tunga sentensi moja na uonyeshe kwa mstari: (al.3) (i) Shamirisho kipozi …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) Shamirisho kitondo …………………………………………………………………………………………………..…… (iii) Shamirisho ala/kitumizi …………………………………………………………………………………………………..…… (o) Tungia vitenzi vifuatavyo sentensi katika hali zilizobanwa; (al.3) (i) Fa (mazoea) …………………………………………………………………………………………………..…… (ii) La (kutendeka) …………………………………………………………………………………………………..…… (iii) Pa (kutendea) …………………………………………………………………………………………………..…… (p) Tambulisha kishazi tegemezi na kishazi huru. (al.2) Wanafunzi waliofanya vyema walituzwa jana. …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… (q) Pambana viambishi mbalimbali katika sentensi ifuatayo. (al.3) Waliwapendezea …………………………………………………………………………………………………..…… …………………………………………………………………………………………………..…… MUHTASARI2. MUHTASARI
Soma taarifa hii kisha ujibu maswali Sisi vijana wa Kenya inatupasa tuwajibike kufanya kazi kwa bidii na kwa dhati ya mioyo yetu uweze kupata ufanisi na uwezekano wa kuinua nchi yetu changa katika kiwango cha juu. Tukumbuke, “Ajizi ni nyumba ya njaa.” Kwa hivyo basi haifai kulaza damu ikiwa matatizo nchini mwetu yametuzonga. Lazima tofanye kazi kwa busara, adabu njema na jitihada kwa moyo mmoja. Sharti tutilie maanani zaidi elimu ya vijana na watu wazima, kilimo, uchumi na amani katika nchi yetu. Tunahitaji taifa la watu walioelimika, kwani bila elimu itakuwa vigumu sana kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo. Tupende tusipende lazima tuzidishe mazao shambani, kwani kila kukicha idadi ya watu inaongezeka. Ni sharti tuweze kujitosheleza katika vyakula. Zaidi ya hayo lazima tujishughulishe na biashara ambapo kwa sasa ni wakenya wachache sana ambao wanatambua umuhimu wake. Wengi ni wale wenye mawazo kwamba lazima aajiriwe maishani. Yatupasa tujitahidi kuleta uchumi katika mikono ya wananchi wa Kenya badala ya kuwaachia wageni. Mafunzo tunayopata nyumbani, shuleni na hata katika jamii, lazima yatuwezeshe kutambua mbinu za kupitia. Tunahitaji elimu tambuzi ambayo itamfanya mwana Kenya kujua wajibu wake katika jamii. Tumesinywa na elimu pumbao; inayo tumbaza na kufanya tusione mbele. Sisi vijana tukiwa viongozi wa siku zijazo tuwe kielelezo chema kwa wengine. Watu wazima washirikiane na kufikiria kwamba wao ni wamoja, “utengano ni uvundo” lugha ya kitaifa ndicho chombo cha pekee ambacho kinatuunganisha na kuwaza kutuwasilishia mapendekezo, mawaidha na hisia zetu. Kukosa ndiko kibinadamu, wakati tunapokosea na kufanya masahihisho. Mara moja kwani; “usipoziba ufa, utajenga ukuta”. Tusikasirike kwa sababu tumesahihishwa makosa yetu na wenzetu. Lazima tujitoe mhanga na kupigania nchi yetu tukiwa wazalendo halisi. Sisi tukiwa vijana sharti tujishughulishe na kuyaangalia matatizo ya nchi, pia kutafuta njia za kutatua matatizo hayo. Siku zote tutekeleze nidhamu. Ni jambo la kusikitisha kwamba sisi vijana twashtumiwa mara kwa mara kwa kutokuwa na nidhamu shuleni na majumbani mwetu. Utamaduni wa asili unakariri sana kuwa tuwe na nidhamu shuleni na nyumbani mwetu. Ili watu waweze kuishi maisha bora na kuwa na maendeeo, amani na upendo; lazima tuwe na bidii, ushirikiano mwema na kuchagua viongozi wenye mioyo ya maendeleo, tukiwa viongozi ambao hawajishughulishi na maendeleo, basi tutabaki nyuma kama mkia siku zote. Bahati mbaya ni kwamba wananchi wengi siku hizi huchagua viongozi wao kwa kufuata ukoo ama utajiri wake. Kwa hivyo basi tuchagueni viongozi ambao watatuletea ufanisi badala ya viongozi wanaotokana na nasaba au utajiri. (a) Dokeza mambo muhimu yaliyomo katika aya ya kwanza.(maneno 65-70) (al 8,2 utiririko) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………..… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………..… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… (b) Fupisha aya ya mwisho kwa kuzingatia mambo muhimu yanayopasa vijana kufanya. (maneno 35- 45) (ala 4, 1utiririko) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………..… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………………..… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… ………………………………………………………………………………………………………..…… ..…………………………………………………………………………………………………………… UFAHAMU1. UFAHAMU (ALAMA 15)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali. Mtoto anapozaliwa huwa ni malaika wa Mungu, hutaraji kuongozwa kwa kila njia ili awe mwana mwelekea. Jukumu la kulea mtoto huanzia nyumbani. Wako baadhi ya watu ambao wanaamini kuwa jukumu hili muhimu hutekelezwa bora na mama; wengine husema ni jukumu la baba. Ni kweli kwamba mtoto huwa na mama yake kwa muda mrefu zaidi ya baba lakini kivuli cha baba hakikosi kumwandama na kumwathiri maisha yake. Uongozi wa mama huanzia siku ya mwanawe kuingia ulimwengu kwa hivyo, mama zaidi ya baba huwa ndiye chanzo cha chemichemi ya maisha ya mwanawe. Mtoto wa kawaida ana tabia ya kuiga kila jambo analoliona na kusikia na mambo ya awali ajifunzayo kutokana na mamaye. Je; mtoto huiga kutokana na mama pekee? Kila utamaduni hasa huku kwetu Afrika, una taratibu zake zilizopangwa kuhusu malezi ya watoto. Kwa mfano ; akina baba wengine wanaoishi maisha ya kijadi huonelea kwamba ni jukume lao kuwalea watoto wa kiume. Kwa hivyo mvulana anayekulia katika mazingira haya akishachuchuka kiasi cha kujua lipi zuri na lipi baya huanzia kuwa mtoto wa baba zaidi ya kuwa wa mama. Baba huathiri mtoto wake kwa kushauri kuhusu maneno ya kiada ya wanaume. Hupenda kukaa naye katika uga wake kwa kumshauri kuhusu maneno ya kiada ya wanaume huku akimkataza kukaa jikoni na kumsisitizia kuwa wanawake ni tofauti naye. Aidha, humfunza sifa kama vile ushujaa na uvumilivu kwa namna ambavyo huona kuwa ni ya kiume. Pindi mtoto anapoonyesha tabia za kikekike, baba hujiandaa kuzitadaruki kwa kumkaripia. Baba hutaka kujiona mwenyewe katika hulka ya mwanawe. Baba kama huyu humpa nafasi ndogo sana mkewe ya kumwongoza mtoto wake wa kiume kwa jambo lolote hata kama wakati mwingine ni la heri. Kwa upande mwingine baba huyu huwa na machache ya kuzungumza na bintiye kwa kuwa huona kuwa sistahili yake kufanya hivyo. Mtoto wa kike huachiwa mamake lakini kutokeapo jambo la kulipima mama huona linampita kimo, humwita baba kuingilia kati na angalabu baba naye humwagiza dadake aje atoe suluhisho mwafaka. Ulezi kama huu una nafasi yake katika jamii, lakini ni lazima tukiri kuwa pia unaendeleza maisha ya fawaishi na kuanzia taasubi ambayo hatima yake ni mwanamke kukandamizwa na mwanaume. Wazazi walio na mwelekeo huu katika malezi yao hufikiri kuwa wataishi na watoto wao katika mazingira finyu na kwa hivyo waendelee kuwapulizia pumzi za kuhilikisha. Lakini ni sharti wakumbuke kuwa wao si walezi peke yao na mtoto hawezi kuishi pekee yake na kuwa na tabia ya kipekee. Leo ataishi kwao lakini kesho itambidi atoke aone ulimwengu. Kila atakapotia mguu ataona mambo mapya yatakayompa tajriba mpya na mawazo mapya ambayo aghalabu yataendelea kuathiri hulka yake. Iwapo tabia alizopata kwa wazazi wake hapo awali zilikuwa na misingi isiyokuwa madhubuti na mielekeo finyu, zinaweza kuwa pingamizi katika maingiliano yake na watu wengine. Mambo haya yanatuelekeza katika kufikiri kwamba maisha ya sikuhizi hayaruhusu ugawaji wa kazi ya malezi ya namna baba na mama wa kijadi. Baba na mama ni walezi wa kwanza ambao kwa pamoja wanapaswa kuelekeza watoto wao katika maisha ya ulimwengu iliyojaa bughudha na ghuhuri. Ni lazima wazazi watambue tangu awali kuwa katika malezi hakuna cha ubaguzi. Hakuna, mambo ajifunzayo mtoto wa kiume ambayo hayamhusu mtoto wa kike. Uvumilivu, bidii, utiifu na kadhalika ni sifa zinazomwajibikia kila mtoto kama vile upishi, ukulima na usafi. Mwanamke tangu azali ameumbwa kuwa mama na haipasi kulazimishwa kuchagua baina ya mtoto wa kike na wa kiume. Mapenzi na wajibu wa wazazi yapaswa yasiwe na mipaka bali yawe maridhawa kwa watoto wote. Maswali (a) Toa kichwa mwafaka cha makala haya. (al.1) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… (b) Kulingana na kifungu hiki, taja mambo mawili ambayo yanaweza kuwa hatari kwa malezi ya watoto. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………..…… (c) Kwa nini baba humpa nafasi ndogo sana mkewe ya kumwongoza mtoto wa kiume katika jambo lolote hata kama wakati mwingine ni la heri. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… (d) Eleza mambo mawili ambayo ni ya manufaa katika ulezi wa jadi. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… (e) Kulingana na makala haya, ushahidi gani unaonyesha kwamba kutegemeana katika ulezi jadi? (al.3) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… (f) Taja sifa mbili ambazo baba humfundisha mwana wa kiume. (al.2) …………………………………………………………………………………………………..…… …..…………………………………………………………………………………………………… (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu hiki: (i) chanzo cha chemichemi… …..…………………………………………………………………………………………………… (ii) Akishachuchuka …………………………………………………………………………………………………..…… (iii) Hulka …………………………………………………………………………………………………..…… mazungumzo kati ya Mwalimu mkuu na mzazi1. Andika mazungumzo kati ya Mwalimu mkuu na mzazi kuhusu chanzo, matumizi na athari za dawa za kulevya miongoni mwa vijana wengi wa siku hizi. 2. Hakuna kizuri kisichokosa ila. Thibitisha methali. 3. Fafanua hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa ili kukabiliana na janga la umaskini hapa nchini. 4. Nilikuwa nimelala fo!fo!fo!nilipogutushwa na kishindo kikuu kutoka upande wa mjini…. 1. (a) Chanzo
(i)Mshawasha kutoka vijana wenzao (ii)Kukosa kazi/ajira (iii)Vyombo vya habari (iv)Kuiga wazazi na wakubwa wao (v)Ukosefu wa maelezo yanayofaa kuhusu athari za dawa hizi Matumizi
Athari
2. Mwanafunzi asimuliw kisa kinachoafikiana na methali hii k.m. mtu aliyekuwa mwema sana lakini hatimaye akapatikana na dosari iliyomfedhehesha sana. Aidha mwanafunzi anaweza kusimulia visa mbalimbali vinavyothibitisha methali hii. 3. Hatua zifaazo ni ;
4. Mwanafunzi aendeleze dondoo hili (mdokezo) kusimulia kisa kinachoafikiana na mdokezo huu. KUANDIKA RIPOTI1. Umeteuliwa kama katibu wa tume ya uchunguzi kuhusu vyanzo vya baa la njaa nchini Kenya. Andika ripoti yako. 2. Ufisadi umekuwa saratani katika nchi nyingi zinazoendelea barani Afrika. Jadili mifano mbalimbali ya janga hili na jinsi ya kulitatua. 3. Mchumia juani hulia kivulini. 4. Mlango wa nyuma ulibishwa mara tatu, Ngo! Ngo! Ngo!. Kufungua tu, nikasikia sauti, “ Lala chini¬¬¬......................” (Endelea). MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA
1. Insha hii ni ya kiuamilifu kuhusu ripoti, sura ya ripoti kuzingatiwa. (i) Kichwa/Anwani (ii) Utangulizi (iii) Matokeo ya utafiti/uchunguzi/mwili – vijisehemu vidogovidogo (iv) Mapendekezo kuhusu matokeo (v) Hitimisho;maoni ya kamati (si ya Katibu) (vi) Sahihi na tarehe/cheo Vyanzo vya baa la njaa • Ukame • Matumizi/utegemezi wa vyakula vya aina moja • Njia mbovu/duni za kilimo • Uzembe/uvivu • Idadi kubwa ya watu • Watu kuhamia mijini – kupuuza kilimo • Ufisadi – sakata mf – ya mahindi • Njia duni za kuhifadhi vyakula • Hali duni za uchukuzi • Kukosa ardhi (uskwota) Ondoa alama 4 za sura ikiwa haijitokezi – akikosa vipengele 4 kati ya 6 (-4s) Ondoa alama 2 za urefu ikiwa haukuzingatiwa Hoja inapomalizikia ipigiwe mkwaju / ionyeshwe kwa mkwaju. 2. (a). Mifano - Barabarani - Ofisini - Mahakamani - Bungeni - Shuleni - Viwandani - Serikalini - Vijijini - Nyumbani Njia za kutatua - Kuunda tume za kukabiliana na ufisadi - Kulipa mishahara mizuri - Kufunza maadili shuleni - Kutumia dini/mahubiri - Kubuniwa kwa sheria kali - Viongozi wawe mifano mizuri ya uadilifu - Uwajibikaji kazini - Viongozi watangaze mali yao hadharani 3. Maana – Kisawe cha mgaagaa na upwa hali wali mkavu. Anayesumbuka kufanya kazi fulani atanufaika hatimaye • Iwe na kichwa – ingawa si lazima • Maana na matumizi ya methali – si lazima • Kisa/visa – Lazima • Hitimisho – Si Lazima • Mtahiniwa ashughulikie pande mbili za methali vilivyo. Atakayeshughulikia upande mmoja tu asipite C+ (Alama 10) • Atakayepotoka atuzwe D Alama 3 20 • Akitoa maelezo ya moja kwa moja bila kisa/visa amepotoka: D 03 20 4. Mtahiniwa aanzie maneno aliyopewa • Kisa kioane na maneno - Kisa cha kutisha mf. Jambazi, wahuni au askari • Asiyeanzia maneno aliyopewa amepotoka D 03 20 • Atakayeongeza kianzio chake lakini asizidishe maneno matano aondolewe alama 2. • Mtahiniwa ni lazima atumie nafsi ya kwanza na ajihusishe; asipojihusisha amepotoka:. D 03 ISIMU JAMII3. SEHEMU D: ISIMU JAMII (Alama 10) a) Eleza majukumu manne yanayotekelezwa na lugha katika jamii (alama 4) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… b) Lugha huchangia vipi kuleta (i) Utengano katika jamii (alama 3) ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Utangamano katika jamii (alama 3) ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… SEHEMU D: ISIMU JAMII
a) i) Kuwasiliana / kupasha habari ii) Hukuza na kuhifadhi utamaduni iii) Hueleza chimbuko la binadamu iv) Kuelimisha / misingi ya mafundisho shuleni v) Kufundisha maadili vi) Kusuluhisha migogoro vii) Hubainisha lengo zuri na baya katika mawasiliano b) Utengano katika jamii i) Ikiwa lugha inayotumika haieleweki kwa wote wanohusika ii) Ikiwa lugha inayotumika husababisha mafarakano, ugomvi na chuki, yenye kuvunja moyo. iii) Ikiwa lugha si dhahiri / wazi – maneno hayaeleweki / hayaleti maana waziwazi. iv) Ikiwa lugha imejawa na kejeli, dhihaka na usemaji kwa mafumbo na yenye utusani. c) Utangamano katika jamii i) Lugha inaeleweka na wote waliopo ii) Lugha inaleta matumaini iii) Lugha haina utusani iv) Ikiwa lugha inayotumika inadhihirisha maana, bila kuhitaji ufafanuzi mwingi. MATUMIZI YA LUGHA (Alama 40)a) Eleza matumizi ya kiambishi ‘ka’ katika sentensi hizi ( alama 3) (i) Juma alikuja akachukua kitabu akaondoka ……………………………………………………………… (ii) Mti ulikatika ukaanguka ……………………………………………………………… (iii) “Nyanya anashona nguo”.Hamisi akasema ………………………………………………………………………… b) Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya jedwali (alama 4) Watoto wale wanafanya kazi lakini wazazi wao wanazungumza nyumbani. ……………………………………………………………………………………… c) Unda nomino kutokana na vitenzi hivi ( alama 2) (i) Onea …………………………………………………………………………… (ii) Umia …………………………………………………………………………………… d) Akifisha sentensi ifuatayo (alama 2) Tulifika tukaagana na mjomba hamisi aishiye mombasa …………………………………………………………………………………………… e) Kwa kutoa mifano mwafaka, eleza tofauti baina ya dhana zifuatazo (alama 4) Sauti ghuna na sauti sighuna ……………………………………………………………………………… f) Onyesha kiima, yambwa, na yambiwa, katika sentensi hii (alama 3) Mwanafunzi alimfutia mwalimu ubao ………………………………………………………………………… g) Andika sentensi hii kwa usemi wa taarifa (alama 2) “Lo! Kube wazuri hawajazaliwa,” Omari alisema baada ya kumwona kisura huyo. ……………………………………………………………………… h) Tunga sentensi moja moja kudhihirisha matumizi ya (alama 2) i. Posa ……………………………………………………… ii. Poza ……………………………………………………… i) Andika sentensi zifuatazo katika hali zilizo kwenye mabano (alama 4) i. Kijikombe chake kilivunjika baada ya kuangukia kijiwe (ukubwa) ………………………………………………………………………… ii. Mtu yule haachi kuandamana na mbwa wake aliyedhoofika kisiha (udogo) ………………………………………………………… j) Eleza maana mbili zinazotokana na sentensi ifuatayo (alama 4) Mtoto alitimua mbio, kuona nyoka …………………………………………………………………………… k) Andika sentensi ifuatayo katika kauli ya kutendesha (alama 2) Nguo zote zimekaushwa na jua …………………………………………………………………………… l) Tunga sentensi kudhibitisha mwingiliano wa maneno yafuatayo (alama 2) Nomino kuwa kivumishi …………………………………………………………………………………… m) Andika kwa wingi (alama 2) Kuwepo kwa mshauri wake kulimfurahisha waziri ……………………………………………………………………………… n) Geuza sentensi ifuatayo katika hali ya mazoea huku ukiondoa -amba (alama 2) Mtoto ambaye alikula ndiye ambaye alilia ……………………………………………………… o) Kamilisha methali ifuatayo (alama 1) Asiye na nadhari… ……………………………………………………… p) Eleza maana ya msemo huu (alama 1) Kwenda mbago… …………………………………………………………… MWONGOZO
a) i) Mfululizo wa vitendo wakati uliopita
ii) Hali ya kutendeka / kuwezekana kwa jambo iii) Katika usemi halisi (Alama 3) c) i) Maonevu, kuonea (kitenzi jina) ii) Umio, maumivu (Alama 4) d) Tulifika, tukaagana na mjomba Hamisi aishiye Mombasa. (Alama 2) e) i) Sauti ghuna zinapotamkwa husababisha kutikisika kwa nyuzi za glota km /b/, /g/, /w/. ii) Sauti si ghuna zinapotamkwa, nyuzi za glota hazitisiki kg /ch/, /sh/, /h/, /l/, /n/. (Alama 4) f) Mwanafunzi – Kiima Ubao – Yambwa Mwalimu – Yambiwa (Alama 3) g) Omari alishangaa baada ya kuona kisura yule kuwa wazuri hawakuwa wamezaliwa Baada ya kumwona kisura yule, Omari alishangaa kuwa wazuri hawakuwa wamezaliwa (Alama 2) h) Posa – Maombi ya kuoa Poza – Tuliza / poesha (Alama 2) i) i) Kombe lake lilivunjika baada ya kuangukia jijiwe (Alama 2) ii) Kijitu kile hakiachi kuandamana na kijibwa chake kilichodhoofika kisiha (Alama 2) j) i) Alikimbia kwenda kuona nyoka ii) Alikimbia alipoona nyoka (Alama 4) k) Jua limekausha nguo zote (Alama 2) l) Nomino kuwa kivumishi Kijana mkulima alituzwa (Alama 2) m) Kuwepo kwa washauri wao kuliwafurahisha mawaziri (Alama 2) n) Mtoto alaye ndiye aliaye ( Alama 2) o) Asiye nadhari siandamane naye (Alama 1) p) Kuenda kandokando (Alama 1) UFUPISHO (Alama 15)Vipindi mbalimbali vya historia vimeshuhudia kuibuka kwa magonjwa ya ajabu. Magonjwa hayo yamewahangaisha watu na kuzishughulisha bongo za wanasayansi na madaktari katika kutafuta tiba. Magonjwa kama vile tauni, kifua kikuu, homa ya matumbo na ndui ni baadhi ya yale yaliyotisha sana nyakati fulani za historia ya binadamu. Magonjwa haya yaliwauwa maelfu ya watu na kuibua mifumo na taratibu za maisha ya watu. Hata hivyo , magonjwa hayo yaliweza kuchunguzwa na kutafutiwa tiba kabla ya kumaliza kabisa kizazi cha binadamu. Lakini hii ni baada ya kuwasukuma maelfu ya watu kaburini. Ulimwengu wa sasa unashuhudia janga jingine la maradhi sugu ya ukimwi. Neno ‘UKIMWI’ lilitolewa kutokana na athari za ugonjwa huo mwilini. Neno “UKIMWI” humaanisha ukosefu wa kinga mwilini, ambapo herufi za kwanza za maneno matatu ziliunganishwa pamoja na kuunda neno hilo. Ugonjwa huu ambao tayari umewaua mamilioni ya watu kote ulimwenguni unazidi kuenea kwa kasi, mfano wa moto katika kicheka. Kutokana na kasi yake ya kuua watu, ugonjwa wa UKIMWI umepewa majina kama vile “umeme” na pia “ugonjwa wa vijana”. Watu wengi wanaoambukizwa virusi vya UKIMWI ni wale walio na miaka kati ya 15 hadi 49. Kundi hili kwa kweli ndilo linalohesabiwa kuwa na nguvu za kutunza jamii kwa njia nyingi. Iwapo wengi katika kundi hili watakumbwa na maradhi haya, watasalia wakongwe na watoto wachanga wasioweza kujimudu. Nchini Kenya, UKIMWI uligunduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka wa 1984. Kufikia mwezi wa Juni 1996, inakisiwa kuwa ugonjwa huu ulikuwa umewaua watu wapatao 65,647 nchini. Hivi sasa, inasemekana kuwa takribani watu zaidi ya 500 hufa kila siku nchini Kenya kutokana na janga hili. Aidha, imedhibitishwa kwamba takriban watu milioni mbili unusu tayari watapoteza maisha yao kutokana na kuaambukizwa virusi vya ugonjwa huu humu nchini. Maradhi haya sasa yamekuwa janga la kitaifa. Kutokana na kuongezeka kwa visa vya UKIMWI, hospitali na zahanati nyingi kote nchini zinashindwa kukidhi mahitaji ya wagonjwa. Kwa hivyo, makundi ya kujitolea na mashirika mbalimbali yameundwa ili kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI. Baadhi ya makundi hayo hutoa tiba ya kisaikolojia pamoja na kuwapa ushauri wa hima ya kuishi, badala ya kukata tamaa. Wagonjwa wengi pia huishia kutibiwa nyumbani kwao. Ugonjwa huu umeathiri jamii kwa njia nyingi. Hali ya maisha na woga, ukosefu wa matumaini, ongezeko la mayatima na kuzorota kwa uchumi kutokana na kutoweka kwa kizazi chenye nguvu za kutoa huduma kwa jamii, na baadhi ya athari za maradhi haya. Lakini jambo la kuzingatia ni hili, tujifunze kutokana na historia.Tuwe na matumaini kwamba siku moja, tiba ya ugonjwa huu itapatikana. Hii ni kwa sababu tumethibitishiwa haya kutoka katika historia yetu wenyewe. Ikiwa magonjwa yaliyosababisha vifo vya wengi kutokana na ukosefu wa tiba yalitokomezwa kupitia juhudi za kimatibabu, sembuse huu ugonjwa tulio nao sasa? Huku tukijikinga kutokana na maradhi haya, tusife moyo bali tuwe na matumaini kwani subira hufuta heri. a) Kwa kutumia maneno yako mwenyewe na bila kupoteza maana, fupisha aya nne za mwanzo (maneno 90 - 100) (alama 3 kwa mtiririko) (alama 12 ) Nakala chafu/maadalizi ……………………………………… Jibu ……………………………………………………………… b) Eleza mambo yanayoleta matumaini kwa wagonjwa wa ukimwi kulingana na aya tatu za mwisho (maneno 40- 45) (alama 1 kwa mtiririko) Nakala chafu …………………………………………………… Nakala Safi ………………………………………………………………… MWONGOZO
UFUPISHO a) i) Vipindi mbalimbali vya historia vimeshuhudia kuibuka kwa magonjwa ya ajabu- tauni, kifua kikuu, homa ya matumbo n.k. ii) Magonjwa haya yamewahangaisha watu na kuzishughulisha bongo za wanasayansi na madaktari katika kutafuta tiba. iii) Magonjwa haya yaliwaua maelfu ya watu na kutibua mifumo na taratibu za maisha ya watu / yaliwaua watu wengi. iv) Magonjwa hayo yaliweza kuchunguzwa na kutafutiwa tiba. v) Ulimwengu wa sasa unashuhudia janga jingine la maradhi sugu ya ukimwi. vi) Ukimwi unazidi kuenea kwa kasi. Umewaua mamilioni ya watu kote ulimwenguni. vii) Ukimwi unazidi kuenea kwa kasi ulimwengu (lazima wazo la kazi litokee). viii) Wengi wa walioambukizwa ni kati ya miaka 15 – 49 ix) Kundi hili lina nguvu / linatunza jamii / wanaosalia ni watoto na wakongwe wanaoachwa. x) Ukimwi uligunduliwa Kenya mwaka wa 1984 (lazima ataje Kenya). xi) Watu zaidi ya 500 hufa kila siku xii) Ukimwi sasa ni janga la kitaifa. b i) Mashirika na makundi ya kujitolea kuwahudumia wagonjwa ii) Makundi hutoa tiba ya kisaikolojia na kuwapa ushauri na hima ya kuishi badala ya kukata tamaa. iii) Wengi hutibiwa nyumbani kwao. iv) Matumaini ya tiba kutokea. Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yoteMgomo uliingia siku ya tano. Asubuhi hii ilikuwa mbaya. Watu mbalimbali walikwisha kamatwa mjini na shamba, wakiwemo wote waliohudhuria kikao maalumu kibandani mwa Fumu. Siku ya pili ya mgomo, Makame aliuawa upenuni pa kibanda chake.Alipatikana amechomwa visu vitano vya mbavu. Mauaji ya kikatili lakini hayakuwa ya siri. Boga, yule kijana aliyehudhuria kikao cha pamoja na Fumu, ambaye toka mwanzo hadi mwisho wa kikao hakusema lolote, saa sita za usiku, aliingia kibandani na kumchopeka Makane visu mbele ya mkewe na wanawe, kisha aliikokota maiti na kuitupa upenuni. Asubuhi, Boga alikuwa mtu wa kwanza katika mkumbo mzima. Yeye alikamatwa kwa uuaji, makosa makubwa zaidi kuliko wenzake. Kukamatwa kwa watu hakukusaidia kitu - mgomo uliendelea. Kule shamba, vilio vya wanawake walioachwa pweke vilisikika. ‘Maskini mume wangu ….maskini, bora, bora ungaliwapeleka hao ng’ombe wakapigwa sindano; kufa kwa ng’ombe si kufa kwa nafsi yako,’ alilia bibi mmoja. ‘Ee, kufa kwa wengi arusi ndugu yangu we. Mimi nimelia we, hata macho yamenivimba kwa mume wangu; ati kakataa kupeleka mazao mjini na kuwajibu askari ufidhuli, lakini halafu nimeona haina maana kulia. Bora tufunge vibwebwe na sisi tuwasaidie kucheza ngoma - wafugaji mia wamekamatwa, wakulima mia mbili na hamsini, na bado wanaendelea kukamata, mji umebaki na wanawake tu; lakini watu wenyewe wana vioja, wanapochukuliwa utawaona wanacheka, sisi tulie nini?’ Mjini kulikuwa na vilio vyake. ‘Mwanangu wamemchukua , wanasema watamfunga au watamwua, kafanyaje? Daima kawatumikia , kapoteza nguvu zake juu yao na sasa…’Alimnung’unikia bibi mmoja. ‘Nini bibi we, wachukuzi na makuli watapata haki zao, na wale wanaozurura iko siku wataajiriwa na watakuta mambo mazuri, na wafanyikazi viwandani watachoka kufukuzwa ovyo ; hivyo ndivyo alivyonambia mwanangu alipokuwa akitoka, pingu mikononi. Nililia bibi, uchungu wa mwana unaujua bibi yangu, lakini baadaye nilipofikiri, nikachanganyisha na yale aliyokuwa akaniambia Ali mwanangu, kila siku; niliuhisi uzito wa maneno yake, nikafuta chozi babu.’ Wasaliti walikuwepo, lakini nafasi ya kusaliti haikupatikana. Kwenye lango la bandarini makuli na wachukuzi walisimama imara na marungu na mapanga tayari kuwang’ariba wahaini wowote. Ng’ambo, vikundi vilitawanyika na kufanya kazi; Wengine walitembea mipini mikononi, tayari kumtia adabu yeyote aliyetokwa na imani ya mgomo. Kikundi kingine kiliwekwa sokoni. Hakuna kitu kilichoingia wala kilichotoka. Magari hayakuwa na safari za shamba wala mjini. Askari walitembea ovyo na kumkamata waliyetaka kumkamata, lakini hakukutokea ghasia wala kupigwa mtu. Mgomo uliendelea, ukimuathiri kila mtu, lakini wale waliodai haki zao hawakuvunja kani. ( Dunia Mti Mkavu-Saidi Ahmed Mohamed) MASWALI 1. Toa anwani mwafaka kwa makala haya. (alama 1) ………………………………………………………………… ……………… 2. Thibitisha kuwa asubuhi hiyo ilikuwa mbaya. ( alama 1) …………………………………………………………………… ………… 3. Mauaji ya Makame yalikuwa ya kikatili. Eleza. (alama 4) …………………………………… …………………… 4. ‘Kufa kwa wengi arusi’. Thibitisha ukweli wa methali hii kwa kurejelea taarifa uliyosoma.(alama 4) …………… ………………………………… … 5. Watu walikamatwa kwa nini? (alama 2) ………………………………………………………… 6. Kwa nini wasaliti hawakupata nafasi yao kusaliti ? (alama 2) ………………………………………………… 7. Eleza maana ya (alama 2) i) makuli …………………… ii) Ukimuathiri ………………………… majibu
MAJIBU
INSHA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA 1. Mtahiniwa azingatie yafuatayo; Mbinu za kupambana na ufisadi -Kuelimisha wananchi kuhusu madhara ya ufisadi kupitia kwa redio, magazeti, runinga n.k. -Kuwaadhibu wahusika – wapelekwe mahakamani na wafungwa jela. -Wananchi waadilike (wawe na maadili mema). -Viongozi wawajibike katika kazi zao. -Sheria za kupambana na ufisadi zibuniwe na kutekelezwa. -Kubuni nafasi zaidi za kazi -Kuimarisha elimu -Kuongeza mishahara kwa wafanyikazi -Tume zaidi za kukabiliana na ufisadi zibuniwe. SURA YA MAHOJIANO -Insha iwe na kichwa kinacholenga mada -Kuwe na mhoji na mhojiwa -Njia ya maswali na majibu -Njia ya kitamthilia ufuatiwe kwa mfano; Juma: Bakari: TAHADHARI -Atakayefululiza bila kufuata mtindo wa mahojiano aondolewe alama (4) sura baada ya kutuzwa. 2. i) Kilimo cha mboga ii) Upanzi wa miti iii) Utengenezaji wa matofali na kuyauza. iv) Ukarabati wa barabara v) Kushirikiana na polisi katika kutoa usalama kwa umma. 3. Maana ya methali Ikiwa umekwisha jitayarisha kufanya jambo, basi bora ulikabili / ulifanye na ulimalize. -Mtahiniwa aandike kisa kitakachothibitisha ukweli wa methali. -Aonyeshe mtu aliyeanza jambo licha ya vikwazo / matatizo, alijibidiisha kulikamilisha. 4. Sharti mtahiniwa aanze insha kwa maneno aliyopewa bila kubadilisha wala kuongeza. Insha ionyeshe harakati za kumtafuta baba mzazi Asimulie jinsi alivyotambua / alivyokutana na babake kwa mara ya kwanza. Hisia alizozipata kv. Furaha / chuki Iwapo mkutano huu ulifaulisha maisha yake ya usoni au la. Ugunduzi wake ulivyoathiri maisha yake TAZ: Kisa kisimuliwe kwa njia ya kuvutia na kusisimua. ISIMU JAMII4. ISIMU JAMII (i) Eleza maana ya lugha sanifu. (alama 1) (ii) Eleza maana ya lafudhi (alama 1) (iii) Jadili matatizo manne yanayokumba ukuaji wa lugha ya Kiswahili nchini Kenya. (alama 8) ISIMU JAMII majibu
4. ISIMU JAMII Lugha Sanifu (i) Ni ile lahoja iliyochanguliwa na kufanyiwa marekebisho ya kimatamushi, kisarufi, kimaana na kimaandishi ili iweze kutumika katika shughuli rasmi kwa mfano — kiunguja. (ii) Lafundi Matamshi ya mzungumzaji yatokanayo na kuathiriwa na lugha ya kwanza au lugha zilizo katika eneo anamoishi. Al -1 au Matamshi ya sauti za lugha yanayomtambulisha mtu au jamii ya lugha Fulani. (iii) Matatizo manne yanayokumba ukuali wa Iuha ya Kiswahili nchini Kenya. 1. Udhaifu na kutekelezwa kwa sera. 2. Matatizo katika mitaala 3. Matumizi mabaya ya lughaushindani wa lugha nyingine 4. Mielekeo hasi 5. Shule za kimataifa na za kibinafsi 6. Ukosefli wa vyombo rasmi vya kukuza Kiswahili 7. Utafiti 8. Msamiati na istilahi MATUMIZI YA LUGHA(a) Pigia mstari iliko shadda mara mbili kwenye neno hili ili kuleta maana zake mbili tofauti. Eleza maana hizo. (i) Ala …………………………..…… (ii) Ala (alama 2) ……………..…… (b) Unda kitenzi an nomino kutokana na nomino an kitenzi ulichopewa kwa kufuata mfano uliopewa. (c) Andika kinyume cha sentensi ifuatayo ukizingatia maneno yaliyopigiwa mstari. Zilizala ilipotokea wanafunzi walitulia na kuanza kucheka. (alama 1) ..……………………………………………………………………………… (d) Kamilisha jedwali kwa kauli ifaayo. (alama 4 1/2) (e) Tambua na uainishe vitenzi katika sentensi ifuatayo. (alama 2) Kuzaa si kazi, kazi ni kuvyeleza. ......................................................... (f) Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia vielelezo vya matawi. (alama 4) Wengi wataitwa lakini wachache watateuliwa .................................................................. (g) Onyesha hali katika sentensi zifuatazo (alama 1) 1. Mwizi akamatwa mtaani Kondele. ............................................................... 2. Nyumba hufagiliwa asubuhi. ................................................................... (h) Kanusha sentensi ifuatayo. (alama 1) Nimemwona Fuchingo na paka wake. ........................................................................ (i) Tunga sentensi yenye kuhusishi cha ‘A’-Unganifu katika ngeli ya I-I, wingi. (alama 1) ............................................................... (j) Andika katika wingi (alama 1) Zigo la kuliwa halilemei .................................................................... (k) Tambua na ueleze aina ya yambwa katika sentensi zifuatazo (i) Mtoto alipigwa vibaya sana na mamake (alama 2) ........................................................................... (ii) Osama alipigwa risasi na wanajeshi (alama 2) ............................................................ (l) Tumia vitate vifuatavyo kutungia sentensi moja moja ili kutofautisha maana zake. 1. Pango (alama 1) .................................................. 2. Bango (alama 1) ............................................................... (m) Onyesha silabi funge kwenye maneno yafuatayo 1. Baiskeli (alama 1) ............................................................................ 2. Muhtasari (alama 1) .............................................. (n) Taja na utofautishe vikwamizo vya meno. (alama 2) .......................................................................................... (o) Geuza katika usemi wa taarifa “Sitatoka hapa leo bila kunilipa. Uliniambiajana nije leo utanilipa. Mbona tena unataka nije kesho?” Mwajiriwa aliteta. (alama 4) ............................................... (p) Onyesha kishazi huru na tegemezi katika sentensi ifuatayo. (alama 2) Mateka wote waliokamatwa leo watafikishwa mahakamani. ................................................................... (q) Tunga sentensi sahihi ukitumia viunganishi vifuatavyo ipasavyo. (alama 2) (i) Lau ............................................ (ii) Waama ................................................. (r) Pambanua viambishi awali, mzizi na viambishi tamati katika kitenzi. (alama 2) Alituwiaje? ............................................ MAJIBU YA MATUMIZI YA LUGHA
3. MAJIBU YA MATUMIZI YA LUGHA
(a) (i) Ala I Ala I Ala - Tamko la mshangao (ii) Ala / Ala / Ala - Mfhko Wa kubeba ala (b) (i) Kuhukumu / hukumu (ii) Riziki (iii) Husudu / Kuhusudu (iv) Rithi / kurithi (c) Zilizala ilipotokea wanafunzi walibabaika na kuanza kulia. (d) (i) Wangapi? wepi / wapi? gani? (ii) Wangapi? wapi / wepi? gani? (iii) Ngapi? zipi? gani? (e) - Kuzaa - kitenzi jina - Si - t/kitenzi kishirikishi kipungufu - Kuvyeleza - kitenzi jina - Ni - kishirikishi kipundufu / t (g) (i) Hali ya - ka / wakati usiodhihirika / wowote. (ii) Hali ya - hu mazoea (h) Sijamwona Fuchingo wala paka wake. (i) Chumvi, sukari, mvua, chai, njia, asali (j) Mjizigo ya kuliwa hayalemei. (k) (i) Mtoto — Yambwa kitondo (ii) Osama — (a) Yambwa kitondo (b) Risasi - Yambwa ala (1) Pango - Tundu, shimo Bango - Maandishi ya kutangaza, tangazo linalobebwa na waandamanaji, tangazo la kampem (m) (i) Baiskeli - bais (ii) Mukhtasati - muh (n) v - ghuna f - sighuna (o) Mwajiriwa aliteta kuwalkwamba asingetoka hapo siku hiyo bila ya kulipwa kwa sababu aliambiwa siku iliyotangulia kuwa aende hapo siku hiyo alipwe I angelipwa. Alitaka kujua sababu ya kumtaka aende siku iliyofuata I keshoye. (p) Tegemezi - Mateka wote waliokamatwa leo Hutu - Watafikishwa mahakamani (q) (i) Kama - Neno lao sharti liwe mwanzoni mwa sentensi (ii) Kwa kweli (r) A — Kiima / mtendo / Nafsi ya 3 — umoja ii — wakati wakati uliopita njeo, tu — Yamwa / watendendewa Nafsi ya — wingi w — mzizi i— kauli kinyambulishi a — kiishio kimalizio je — kiulizi. Ukiwa mtoto unadhani ulimwengu ni kipande kimoja cha keki kilicho kitamu mithili ya asali.17/12/2023 Jibu makala yafuatayo kisha ujibu maswali.UFUPISHO Ukiwa mtoto unadhani ulimwengu ni kipande kimoja cha keki kilicho kitamu mithili ya asali. Hakuna dhiki, hakuna mateso, hakuna kuhuzunika kwa ama yoyote. Neno huzurn linasikika masikioni kama neno lisiloelekea kwenye uhalisia wowote. Kwa watoto duma imejaa raha, starehe na vcheko visivyoisha. Maisha ni ahadi njema, yenye matokeo ya kufurahisha na kustarehesha tu sio kudhikisha na kuhuzunisha. Huyu tunayemzungumzia hapa ni mtoto mdogo ambaye hajajua kubainisha kitendekacho mkono wake wa kushoto wala idle kinachofanyika hasa katika mkono wake wa kulia. Hata hivyo, jinsi mtoto anavyoendelea kukua na kufahamikiwa na mambo, vigambo na kadhia zinazoendelea katika mazingira yake, anabainikiwa na mengi machungu ambayo huleta huzuni, sb raha. Hebu tuanze na nyumbani kwao mtoto. Aghalabu, watoto wote hupendwa kwao nyumbani, iwapo wazazi wao ni watu wangwana na wana nafasi ya kulea watoto wao bila taabu. Hata hivyo watoto huchapwa pale wanapokuwa watundu, jambo ambalo huwahuzunisha sana, japo ni wajibu wa wazazi sababu, kama isemwavyo, meha mwana kulia hulia yeye. Pili, inajulikana wazi kwamba watoto wengi siku hizi huenda shule. Huko shule, wao hupendelea sana kucheza kuliko kusoma. Iii wasome kama inavyotakikana, m sharti waelekezwe barabara katika njia hiyo na walimu wao. Katika kuelekezwa huku, walimu wanaweza kulazimika kuwaacthibu, hasa wale watoto ambao huzembea na kutofanya kazi zao wanazopewa kufanya nyumbani kama kawaida ya mfumo wa shule ulivyo. Watoto wa ama hii wanapotiwa adabu raha hujitenga na buzuni huwatawala. Huzuni, hivyo basi, maonekana ya kuwa m uso wa pili katika maisha ya wanadamu, uso wa kwanza ukiwa raha. Na kwa hakika wanaohuzunika si watoto peke yao. Kila mtu duniani ni sharti, katika wakati mmoja au mwingine, azongwe na huzuni. Inajulikana wazi kwamba wanadamu wote hawapendi huzuni asilani na hakika kabisa, kila binadamu huchukia huzuni na kustahabu raha. Hata hivyo, raha humjia binadamu kwa nadra sana, ilhali huzuni humvamia wakati wowote, hata akiwa yumo katikati ya kustarehe. Si tu, inajulikana dhahiri kwamba hakuna mtu asiyewahi kuonja huzuni, japo wapo wengi kweli kweli wasiowahi kuonja raha maishani mwao. Zingatia mtoto anayezaliwa, halafu wazazi wake wanaaga dunia, pengine katika ajali, kabla mtoto mwenyewe hajaweza kujikimu. Mtoto huyu anaishi kutegemea jamaa za wazazi wake. Watu hawa wasipokuwa na nafasi wao wenyewe kimaisha pamoja na ukarimu unaohitajika basi mtoto anateseka na kuhuzunika sana katika maisha yake yote. Ama zingatia mtoto anayetupwa na mamake kijana, anayempata bila kupanga. Hata mtoto huyu akiokotwa na kulelewa na wahisani, maisha yake yatakuwa ya taabu, dhiki na huzuni. Au zingatia mtoto anayelelewa na mama wa kambo anayeondokea kuwa mwovu. Mtoto huyu atakayoijua ni huzuni tu. Ama zingatia mtoto ambaye babake ni mievi na analojua ni kurudi nyumbani usiku akiimba nyimbo za kilevi, kuita mkewe kwa sauti kubwa, kuitisha chakula na kufurahia kupiga watoto wote na mama yao ndipo apate usingizi mnono. Mtoto mwenye baba wa ama hiyo atakayoijua ni huzuni tu, si raha asilani. MASWALI (a) Ukitumia maneno yako mwenyewe na bila kupoteza maana, fupisha aya nne za mwanzo. (Maneno-100). (Alama 9) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………… (b) Ukizingatia aya ya mwisho eleza hali mbalimbali zinazowatia watoto buzuni. (Maneno 40-45) (Alama 4) Nakala chafu ………………………………………………………………………………………………… Nakala safi ………………………………………………………………………………………………… Majibu
Majibu (a) (i) Mtoto hudhani/hufikiri ulimwengu umejaa raha na hauna huzuni/hauna mateso/haudhikishi. (ii) Mtoto huyu ni yule mdogo ambaye hajajua kubainisha mambo. (iii) Anavyoendelea kukua, anafahamishwaanabainikiwa na mengi yaletayo huzuni. (iv) Nyumbani ingawa hupendwa, huadhibiwa wanapokuwa watundu na kuhuzunika. (v) Shuleni wanapozembea kazi, wanaadhibiwa na hili huwahuzunisha. (vi) Huzuni basi ni uso wa pili katika maisha ya binadamu, uso wa kwanza ukiwa raha. (vii) Kila mtu duniani huzongwa na huzuni / huhuzunika (viii) Raha humjia mwanadamu kwa nadra ilhali huzuni humuvamia wakati wowote. (ix) Wako watu wengi wasiowahi kuonja raha maishani mwao (Hoja 9-al-1 =9) (b) (i) Mtoto anapofiwa na wazazi (ii) Mtoto anayetupwa na mamake kijana baada ya kuzaliwa. (iii) Mtoto anayelelewa na mama wa kambo mwovu. (iv) Mtoto ambaye babake ni mlevi Hoja4-Al-1 —4 Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.UFAHAMU Wanasaikolojia wanabainisha kati ya sehemu mbili kuu katika akili ya binadamu; ung’amuzi na ung’amuzibwete. Ung’amuzi ni sehemu ya ubongo ambayo kimsingi hupanua na kudadavua yanayotendeka hususan mchana. Ung’amuzibwete ni kibinimethali chake; hufanya kazi wakati binadamu anapolemazwa na usingizi. Baadhi ya mambo anayoshuhudia binadamu mchana yanaingia kwenye ung’amuzibwete wake na kutokeza katika ndoto zake usiku. Kwa mujibu na mawazo ya Sigmund Freud, mwanasaikolojia wa jadi anayechukuliwa na wengi kama mwasisi wa taaluma ya saikolojia, mambo yanayopatikana katika ang’amuzibwete yana sifa hasi. Freud alidahuli kuwa binadamu huyaficha na kuyabania kwenye ang’amuzibwete mambo ambayo hawezi kuyasema kadamnasi. Alieleza kuwa matamanio yasiyokubalika, makatazo ya jamii, fikra na kauli zilizobaramishwa na miko ya kijamii hubanwa katika ang’amuzibwete. Shehena hiyo ndiyo inayochipuza kwa njia ya ishara za ndoto, mitelezo ya kauli, yaani maneno au kauli zinazotutoka bila wenyewe kukusudia, ishara na lugha ya kitamathalu katika uandishi wa kibunifu na kadhalika. Ung’amuzibwete una uwezo mkubwa wa kuathiri matendo ya bmadamu. Huu ndio msmgi unaowafanya wanasaikolojia wengi, ukiwemo Freud, kusema kuwa tajriba ya mtoto maweza kufichwa kwenye sehemu hiyo na hatimaye kuishia kutokeza katika utu uzima wake. Kwa kuwa tunapoingiliana na binadamu wenzetu kila siku tunayang’amua tuyafanyayo, ung’amuzi unaotuwezesha kutambua jema na ovu unatawala. Ung’amuzibwete unapotawala binadamu wenzetu watashindwa kutuelewa. Hii ndiyo hali anayokuwa nayo mwendawazimu. Ung’amuzibwete wake hutawala. Sisi tunaotawaliwa na ung’amuzi tunashindwa kumwelewa; naye bila shaka anashindwa kutuelewa. Carl Gustav Jung, aliyewahi kuwa mwanafiinzi wa Freud, aliupinga mwelekeo wa Freud na kuungalia ung’amuzibwete kamajaa la mawazo mabaya, matamanio, nia, fikira tuli na dhana ambazo ni hasi. Jung alizuka na dhana mbili muhimu: Ung’amuzibwete wa kibinafsi na ung’a,izibwete jumuishi. Alisema mambo, fikra na uzoefu wowote mbaya unaomuhusu mtu binafsi hupatikana katika ung’amuzibwete wa kibinafsi. Dhana ya ung’amuzibwete jumuishi aliitumia kuelezea sehemu ya akili ya binadamu ambayo inamfanya ayatende matendo fulani kama binadamu wenzake licha ya tofauti zao kiwakati na kijiografia. Kwa mfano, binadamu wengi wana sherehe za kuzaliwa mtoto, kuoa, ibada au mviga unaohusiana na kifo licha ya tofauti zao. Jung alisema kuwa kinachochochea hali hii ni urithi Fulani wa kila mwanadamu. Urithi huo unaopatikana katika ung’ amuzibwete una uwezo wa kuathiri ung’amuzi na matendo ya binadamu ya king’amuzi. Wanasaikolojia wanashikilia kuwa binadamu hawezi kukamilika bila kuzuhusisha sehemu zote mbili kwa sababu zinaathiriana. MASWALI(a) Kwa nini ung’amuzibwete unaelezwa kama kinyume cha ung’amuzi? (alama 2) .……………………………………………………………………………………………… (b) Eleza mtazamo wa Freud kuhusu ung’amuzibwete (alama 3) ……………………………………………………………………………………………….. (c) Kwa mujibu wa Freud yaliyomo kwenye ung’amuzibwete hudhihirika vipi? (alama 4) ……………………………………………………………………………………………….. (d) Eleza tofauti ya mawazo kati ya Sigmund Freud na Carl Gustav Jung. (alama 4) ……………………………………………………………………………………………….. (e) Taja hoja inayowafungamanisha Jung na Freud. (alama 2) .……………………………………………………………………………………………… Majibu
(a) Ung’amuzibwete hufanya kazi mtu akiwa amelala/usiku kinyume na ung’amuzi ambao hufanya kazi mtu akiwa macho/mchana. 1x2 = 2 (b) Mambo yanayopatikana katika ung’amuzi bwete (i) Yana sifa hasi / hubana sifa hasi (ii) Huficha mambo ambayo mwanadamu hawezi kuyasoma wazipeupembele ya kadamnasi (iii) Hubana matamanio yasiyokubalika na jamii (iv) Hubania kauli zilizoharamishwa na miiko ya jamii. 1x3= Hojayoyote mojaAl— 3 (c) (1) Kwa ishara za ndoto (ii) Kwa mitelezo ya kauli (iii) Kwa ishara (iv) Kwa matumizi ya lugha ya kitamathali katika uandishi 4x1= 4 AIa,na-4 (d) Freud anawaza kuwa ung’amuzibwete ni jai la mambo hasi ilhali Jung ana dhana mbili kuhusu ung’amuzibwete (i) Ile ya kibinafsi (ii) Ile ya jumuishi au Freud ana mtazamo wa dhana hasi katika ung’amuzibwete ilhali Jung anawaza dhana ya jumuishi. 2x2=4 Mwanafunzi aonyesha dhana zote mbili ya Freud na ya Jung (e) Ung’amuzibwete una uwezo wa kuathiri ung’amuzi na matendo ya binadamu ya king’amuzi. Al-2 Insha
Mwongozo huu unatumika sambamba na mwongozo wa kudumu wa Insha [102/1]
1. Andika hotuba ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kupambana na Ufisadi nchini kwa washika dau wote katika Kaunti ya Kakamega. -Insha ihusishe hoja zisizopungua sita kati ya hizi na nyingine zinazorejelea maswala yoyote ya ufisadi nchini: --Chanzo cha ufisadi k.m. umaskini, tamaa, kuiga wengine, kutaka kuhepa adhabu, n.k. --Kunakotokea ufisadi, k.m. ofisini, hospitali, shuleni, mahakamani, katika vyombo vya usafiri, n.k. --Athari za ufisadi k.m. ufujaji wa pesa, nchi/mashirika kutoendelea, n.k. --Adhabu kwa ufisadi k.m. kushikwa, kufungwa, kufutwa, kulazimishwa kulipia, n.k. --Hatua zinazochukuliwa na shirika lake kupambana na ufisadi. --Mapendekezo yake kwa umma kuhusu jinsi ya kupambana na ufisadi. SURA Ionyeshe kuwa ni hotuba kutokana na kianzio, kinachotambua au kuiamkua haadhira. Pia kiishio. Insha yenyewe iandikwe kwa mtiririko ikitumia nafsi ya kwanza. Adhabu ya kawaida ichukuliwe kwa insha isiyochukua sura inayostahili (-04s) 2. Eleza chanzo cha ongezeko la bei ya bidhaa nchini mwako, huku ukionyesha athari za ongezeko hili. CHANZO --Ufisadi --Tamaa --Shilingi ya Kenya kukosa nguvu dhidi ya Dola ya Marekani.
ATHARI
3. Aiszfuye mvua imemnyea. Ni methali. Insha iwe na kisa (au visa) kinachoonyesha ukweli wa methali. Methali ina maana kuwa anayelizungumzia jambo, kulieleza au kulisifu ana tajriba nab. Insha ionyeshe sifa itolewayo na pia alivyonyewa. 4. “Karne ya 21 imeleta ongezeko kubwa la vyombo tofauti vya habari nchini, pamoja na athari anuwai” Jadili kauli hii. ONGEZEKO Insha ithihirishe ukweli kwamba vyombo vya habari vimeongezeka kwa kutoa mifano ya magazeti, majarida, stesheni za redio, runinga, n.k. atakayejaribu kuipinga kauli hii atakuwa amepotoka. ATHARI Ni nzuri na mbaya • Habari zinapatikana kwa urahisi. • Hakuna usiri usiofaa wa serikali tena. • Kuna burudani tele. • Vinaelimisha. • Watu (hususan wale mashuhuri) wamekoseshwa siri katika maisha yao. • Vyombo vingine vinachochea makabila, n.k. • Kuna ongezeko la picha/habari za ngono. • Maadili yamezorota. • N.K. Insha ihusishe hoja zozote sita au zaidi katiya hizi na nyingine. ZIADA YA JUMLA Tumia mwongozo wa kudumu wa insha ili kutuza insha katika viwango kati ya A+ na D-. hoja katika maswali 1,3 na 4 itambulike kwa mkwaju (‘f) kushoto, pembezoni mwa aya iliyobeba hoja. ISIMU JAMII (Alama10)a) Eleza maana ya istilahi zifuatazo i) Lafudhi (alama 1) __________________________________________________________________________ ii) Pijini (alama 1) __________________________________________________________________________ iii) Lahaja (alama 1) __________________________________________________________________________ b) Eleza njia tatu za kupunguza tofauti za kilahaja (alama 3) __________________________________________________________________________ c) Fafanua sababu zozote zinazosababisha makosa katika matumizi ya lugha ya Kiswahili (alama 4) Mwongozo
a) i) Lafudhi – ni upekee unaojitokeza baina ya watumiaji mbalimbali wa lugha moja. ii) Pijini – ni lugha inayoibuka panapotokea mwingiliano wa watu wanaozungumza lugha tofauti kwa lengo la kurahisisha mawasiliano. iii) Lahaja ni tofauti katika matamshi, maumbo na matumizi ya maneno zitokanazo na tofauti katika maeneo mbalimbali kwa lugha yenye asili moja. b) i) Kusanifisha lugha ii) Kuimarisha njia za usafiri baina ya maeneo ambapo lugha inatumiwa km barabara iii) Kuwepo kwa mfumo mmoja wa elimu ambapo lugha moja inatumiwa iv) Maendeleo ya njia za kupashana habari km simu magazeti, redio n.k v) Kuweka utawala mmoja k.v. muungano wa Afrika Mashariki. c) Lugha ya kwanza Hali – uchovu / ugonjwa wa mzungumzaji Uwili lugha / uwingi lugha Kwa kukusudia km. waigizaji. Kutozingatia ngeli Kutoelewa lugha/msamiati Kutozingatia upatanisho wa ngeli Kutozingatia tahajia/hijai/maendelezo SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (Alama40) a) Tofautisha sauti zifuatazo. (alama 2) /a/ /u/ __________________________________________________________________________ b) i) Ngeli ni nini? (alama 1) __________________________________________________________________________ ii) Maneno haya yamo katika ngeli gani? (alama 2) Tayo __________________________________________________________________________ Kipepeo __________________________________________________________________________ c) Akifisha sentensi hii kwa njia tatu tofauti kuleta dhana tatu tofauti. (alama 3) Babu alimchapa nyanya __________________________________________________________________________ d) Ainisha mofimu katika neno lifuatalo (alama 3) Sikumkaribisha __________________________________________________________________________ e) Andika katika usemi wa taarifa (alama 3) “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim __________________________________________________________________________ f) Andika kwa wastani (alama 2) Magoma hayo yatachezwa mawanjani __________________________________________________________________________ g) Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani h) Tofautisha sentensi zifuatazo. (alama 2) i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri ii) Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri __________________________________________________________________________ i) Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya: (alama 3) a) Kulinganisha __________________________________________________________________________ b) Sababu __________________________________________________________________________ c) Wakati __________________________________________________________________________ j) Kwa kutoa mifano katika sentensi onyesha matumizi mawili ya parandesi (alama 2) __________________________________________________________________________ k) Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo (alama 4) Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana. __________________________________________________________________________ l) Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi (alama 2) i) Nisimamapo huchekwa ii) Ninaposimama huchekwa __________________________________________________________________________ m) Andika sentensi hii upya bila kubadilisha maana ukitumia ‘o’ rejeshi na kiambishi ngeli mwanafunzi alitumwa nyumbani juzi na hajapata karo hadi leo. __________________________________________________________________________ n) i) Eleza dhana ya kishazi tegemezi (alama1) __________________________________________________________________________ ii) Bainisha aina za vishazi (alama 2) Konde iliyopaliliwa ilituletea mazao mengi sana __________________________________________________________________________ o) Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma (alama 2) __________________________________________________________________________ Mwongozo
a) /a/ ni irabu ya kati (hutamkwa kwa kutumia sehemu ya kati ya ulimi) midomo hutandanzwa inapotamkwa. /u/ ni irabu ya nyuma (ulimi huinuliwa juu na kupindwa nyuma ya inapotamkwa. midomo kuviringwa inapotamkwa. b) i) Ngeli ni kundi la nomino za aina moja ii) Tayo – LI – YA Kipepeo – A – WA c) Babu alimchapa nyanya? (swali) Babu alimchapa nyanya! (mshangao) Babu alimchapa nyanya. (maelezo / taarifa) d) si – kiwakilishi cha ukanushaji ku – kiwakilishi cha wakati uliopita m – kiwakilisha cha mtendwa karib – mzizi ish – kiwakilishi cha kauli a – kiishio e) Salim alisema kwamba wangepata mwaliko wao siku iliyofuata au Salim alisema kuwa tungepata mwaliko wetu siku iliyofuata. f) Ngoma hizo zitachezwa uwanjani g) S – KN + KT KN – N + V + N N - Wanafunzi V – wenye N – bidii KT – T + N T – hufuzu N – mtihani h) i) Nge – huonyesha wakati ujao na kuwa kuna uwezekano ii) Ngali – huonyesha wakati uliopita na hakuna uwezekano / ni majuto i) a) Abunuwasi ni mjanja kama sungura Dhahabu ni ghali kuliko shaba b) Juma ametuzwa kwa uhodari wake c) Jogoo huwika kabla ya saa tisa usiku j) Jona (kijana mpole) anasafiri leo kwenda mjini? maelezo ya ziada Aziza (mhusika mkuu) aliomba talaka Mjomba: (akikohoa) habari? – tamthilia / mazungumzo Kufungia nambari (1) (2) (3) k) Nyanya – kiima Mjukuu – shamirisho kitondo Nyumba – shamirisho kipozi Chagizo – i) mwaka jana ii) kwa matofali Shamirisho ala – matofali Alimjengea – kiarifa l) i) Wakati wowote ii) Wakati maalumu m) Mwanafunzi aliyetumwa nyumbani juzi, hajapata karo hadi leo. n) Kishazi tegemezi – ni kundi la maneno lililo na kiima na kiarifa lakini haliwezi kujisimamia pekee kama sentensi. hutegemea kishazi huru ili kupata maana. o) Watoto hao wanachuma machungwa Nondo za madirisha hutengenezwa kwa chuma Mimi ninafanya kazi ili kuchuma pesa Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo HAKI ZA BINADAMU Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa kuwa. Kama binandamu tunaamini njia yetu ndiyo sahihi, yenye mantiki na inayopasa kufuatwa na kila mtu. Msingi huu huu unakwenda kinyume na kutambua kila binadamu ana haki ya kufikiri, kusema au kuongea na kutenda mradi asikiuke haki ya mwenzake iliyo sawa na yake. Nguzo mojawapo inayogongomelea hoja hii ni Haki za Binadamu. Azimio kutangaza Haki Bia za Binadamu liliafikiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Desemba 1948. Baraza kuu hilo liliyasisitizia mataifa wanachama umuhimu wa kuyasambaza, kuenezea, na kusisitiza kusambazwa kwa azimio hilo katika shule na taasisi za kielimu. Msingi wa uhuru, haki na amani ulimwenguni ni kutambua binadamu wote wana haki sawa. Ingawa kimsingi jamii na mataifa yote ya ulimwengu yanapaswa kuthamini, kusambaza na kuhimiza umuhimu wa Haki za Binadamu zipo jamii ambazo hukiuka haki hizo. Matokeo ya ukiukaji huu yana athari hasi sana kama ilivyotokea nchini Rwanda na Bosnia. Herzegovina kulikotokea mauaji ya halaiki. Azimio la Haki za Binadamu linajumuisha vipengele kadha ambavyo ni mihimili mikuu ya Azimio lenyewe. Kipengele msingi kabisa kinasisitiza kuwa kila kiumbe anazaliwa huru na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine. Ukweli wa kauli hii ulikokotezwa na kauli ya mwanafalsafa maarufu Jean Jacques Rosseau aliyesema kuwa kila kiumbe huzaliwa huru lakini huwa katika pingu ulimwengu mzima. Kauli hii ilitambua ukiukaji huu wa kipengele hiki. Kipengele cha pili kinasisitiza kuwa binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia, utajiri au chochote kile. Vipengele vingine vinatukumbusha kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi. Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa au unyonge wa kutumikishwa kwa namna yoyote ile. Suala hili linasisitizwa na kipengele cha sita kinachokataza kudhalilishwa kwa watu au kutunzwa kwa namna yoyote ambayo inamfedhehesha kama kiumbe. Azimio la Haki za Binadamu linasisitiza kuwa binadamu yoyote nyule ana haki ya kupata ulinzi wa kisheria. Binadamu huyo hapaswi kubaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa. Hata hivyo sio watu wote ulimwenguni ambao wanazifurahia haki hizi za kimsingi. Zipo lukuki za jamii ulimwenguni ambako haki za kimsingi zinakiukwa. Katika nchi ambazo zinaongozwa na watawala wa kiimla, si ajabu kuona haki za binadamu zikikiukwa. Viongozi wa aina hiyo huwa wamegeuzwa ng’ombe wa shemere na tamaa, ubinafsi na ukatili usiojua thamani ya utu. Viongozi wa aina hii wanasahau kuwa kila binadamu ana haki ya kuishi maisha huru, asipotumikishwa wala kulanguliwa kama bidhaa. Nchi za kiimla aghalabu huongozwa na itikadi kuwa kiongozi ndiye pekee ambaye ana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda. Watu wengine wanapaswa kumfuata kisilka kama yule mbwa wa Pavlov ambaye alitokwa na mate kila kengele ilipopigwa. Viongozi wa ama hii hawachelei kuwatenza nguvu raia zao: Kuwadhalilisha kwa namna nyingi. Viongozi wa aina hiyo huiona sheria ya nchi kama iliyowekwa kwa watu wengine bali sio wao. Msimamo huu unakwenda kinyume na kipengele cha saba cha Haki Bia za Binadamu kisemacho kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria. Baadhi ya haki zinazokiukwa katika jamii za kimabavu ni haki ya watu kuungana, kuwaza, kushiriki katika maamuzi ya serikali, kuwa mwanachama wa jumuia waitakayo, kumiliki mali, kutembea, kuishi anakotaka kutohukumiwa bila ya kuwako na utaratibu wa kisheria. Ni muhimu hata hivyo kujua ni muhimu kwa raia wenyewe kujielimisha na kuzijua haki zao. Serikali inapaswa kuwa mlinzi wa sheria zenyewe. Lakini muhimu kujua pia kuwa mlinzi naye hulindwa pia. Maswalia) Kwa maneno kati ya 90 – 100 fafanua Haki Bia za Binadamu zilizoafikiwa na Baraza kuu la umoja wa Mataifa. (alama 10) Nakala Chafu __________________________________________________________________________ Nakala Safi __________________________________________________________________________ b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu. (Maneno 50 – 60). Nakala Chafu __________________________________________________________________________ Nakala Safi __________________________________________________________________________ Mwongozo
a) Kwa maneno kati ya 90- 100 fafanua Haki Bia za Binadamu Zilizoafikiwa na Baraza kuu la Umoja wa mataifa Kila kiumbe anazaliwa humu na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine’ • Binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia au chochote kile. • Kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi • Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa, kutumikishwa, kudhalilishwa au kutunzwa kwa namna inayomfedhehesha kama kiumbe. • Haki ya kupata ulinzi wa kisheria • Kutobaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa . Alama 8 utiririko alama 2) b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu • Tamaa ya uongozi • Ubinafsi • Ukatili, hawajui thamani ya utu • Kiburi cha kujiona kuwa wao ndio wanaofahamu mambo zaidi • Husahau kuwa binadamu ana haki ya kuishi maisha huru bila kutumikishwa au kutanguliwa kama bidhaa • Hudhani wao tu ndio wana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda na wananchi wanapaswa kufuata tu • Huona kuwa sheria ya nchi imewekewa wengine na wala sio wao hivyo huwatenza nguvu raia zao Alama 4, utiririko alama 1) Maswali na Majibu ya UFAHAMU (Alama15)Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali Tokea muundo mpya wa serikali ya ugatuzi uanze kutekelezwa miaka miwili iliyopita, kumeendelea kushuhudiwa matatizo mengi hali iliyopelekea kushuhudiwa kwa msururu wa migomo na maandamano ya raia. Fujo za karibuni kabisa ni zile zinazoshuhudiwa katika miji mikubwa za wachuuzi na wafanyibiashara wakipinga hatua za serikali za kaunti kuwatoza ushuru takribani kwa kila huduma na bidhaa ikiwemo wanyama, kuku na ndege. La kuhuzunisha zaidi katika baadhi ya majimbo imeripotiwa kuwa raia wamelazimishwa kulipa ushuru kwa kutaka tu kuona maiti za jamaa zao kwenye vyumba vya kuhifadhi maiti. Wanasiasa wameonekana kuwa na wakati mgumu kutetea mfumo huu mpya wa ugatuzi huku baadhi wakisema kwamba matatizo yanayoshuhudiwa kwa sasa yametokana na ugeni wa mfumo huo. Wengine wameinyoshea kidole serikali ya kitaifa kwamba ndiyo inayosambaratisha muundo huu. Wengine wanahoji kuwa bado ni mapema na kwamba kunatajika muda mrefu ili kufaulu. Ni wazi kwamba kumekosekana nidhamu bora ya kusimamia maisha ya raia nchini Kenya. Matatizo yanayokumba raia kwa sasa ni dalili kuwa mfumo wa serikali ya ugatuzi umeongezea chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu. Swali ni je, hadi lini nidhamu ya kusimamia raia itakuwa ni suala la majaribio na makosa? Hatua ya kuwarundikizia raia ushuru mkubwa ni kitendo cha unyonyaji na cha dhuluma kinachofaa kupingwa. La kufahamishiwa hapa ni kwamba ushuru ndio njia kubwa ya kuzalisha mapato ya serikali zinazojifunga na mfumo wa kimagharibi wa kiuchumi wa kibepari ikiwemo Kenya. Asilimia 90 ya mapato ya serikali za kibepari huegemea ushuru. Kwa hivyo hatua ya serikali za kaunti katika kuwanyonya raia kwa kuwalipisha ushuru si ajabu bali ni thibitisho kuwa jamii ya Kenya inaongozwa na nidhamu ya kiuchumi ya ubepari mfumo wa unyonyaji na ukandamizaji. Ukweli unabakia kuwa ndani ya serikali za kibepari raia ndio hubebeshwa mzigo wa ushuru unaoishia matumboni mwa viongozi! Miito ya mabadiliko ya katiba na ya miundo mipya ya kiutawala si lolote ila ni moja tu ya hatua za mfumo wa kibepari kujipa muda wa kuishi na kuziba aibu zake za kushindwa kusimamia maisha ya watu. Kufeli huku kwa mfumo huu kunashuhudiwa hadi kwenye nchi kubwa za kibepari kama Marekani na Uingereza hivyo nazo zimekumbwa tele na maandamano na fujo za raia wakilalamikia hali ngumu ya maisha. Maswali a) Yape makala haya anwani mwafaka. (alama 1) __________________________________________________________________________ b) Eleza mtazamo wa wanasiasa kuhusu utepetevu wa mfumo huu. (alama 3) __________________________________________________________________________ c) “Ugatuzi nchini Kenya ni mfumo wa kibepari” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea makala. (alama 3) __________________________________________________________________________ d) Migomo ni zao la matatizo yaliyogatuliwa kutoka kuu. Toa sababu nyingine zinazosababisha migomo katika serikali za ugatuzi (alama 4) __________________________________________________________________________ e) Thibitisha jinsi mfumo wa ugatuzi umeongeza chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu (alama 2) __________________________________________________________________________ f) Eleza maana ya maneno yafuatayo (alama 2) i) Ugatuzi __________________________________________________________________________ ii) Kibepari __________________________________________________________________________ MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA (a) Changamoto za Ugatuzi/Matatatito ya tigatuzi/Ugatuzi ( alama 1x1 = 01) (b) - Ugatuzi ni mfumo geni (Alama 3x1=03) - Serikali kuu kutowajibika - Kudai kuwa mfumo huu unahitaji mda zaidi (c) - Mfumo wa ugatuzi nchini umehusisha matendo ya kibepari kama vile; (alama 3x1=03) - Raia kupewa mzigo wa kulipa ushuru ili kuipa serikali mapato - ushuru ndio njia kubwa ya kuzalisha mapato ya serlkal zinazojifunga na mfumo wa kimagharibi wa kiuchumi - viongozi kuwanyonya raia walio maskini (d) - Hali mbaya ya muundo msingi (alama 4x1= 04) - Viongozi kuendeza ufisadi - Ukosefu wa usawa katika ugavi wa rasilimali - Viongozi kupuuza mchango wa wananchi (e) - Raia kulazimishwa kulipa ili kuona maiti za jamaa zao katika fuo (alama 2x1=02) - Raia kurundikiziwa mzigo wa kulipa ushuru mkubwa - Ushuru unaolipwa na wananchi hauwasaidii wananchi la huishia mifukoni mwa viongozi (f) (i) Ugavi wa mamlaka na raslimali kutoka serikali kuu hadi mashinani (alama 2x1 =02) (ii) mfumo wa kiuchumi wa watu wachache kumiliki raslilmali kwa kuwapora wengine Ondoa nusu alama kwa kila kosa la sarufi hadi makosa sita. Ondoa nusu alama kwa kila kosa la tahajia hadi makosa sita. |
Categories
All
Archives
July 2024
|
We Would Love to Have You Visit Soon! |
Hours24 HR Service
|
Telephone0728 450425
|
|
8-4-4 materialsLevels
Subjects
|
cbc materialsE.C.D.E
Lower Primary
Upper Primary
Lower Secondary
Upper Secondary
|
teacher support
Other Blogs
|