Maswali na Majibu KCSE Kiswahili
Ufahamu | Ufupisho | Isimu Jamii | Insha | Utumizi wa Lugha
MATUMIZI YA LUGHA1. MATUMIZI YA LUGHA a) (i) Taja sauti mbili ambazo ni irabu na wakati huo huo konsonanti. (alama 2) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Tambua sauti hafifu kati ya zifuatazo: (alama 1) /K/, /r/, /gh/,/ sh/, /w/ ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… b) Onyesha yambwa tendwa na yambwa tendewa katika sentensi hii. (alama 2) Mbunge wa Mtondo Kaskazini atawajengea wanakijiji josho kisha aghurie mjini. ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… c) Andika kwa msemo taarifa (alama 3) “Sitakwenda sokoni leo ila nitakwenda kesho,” nikamjibu ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… d) Eleza matumizi ya neno wale katika sentensi hii. Wale walioiba ni mabanati wale ambao waliambiwa wale kabla ya kitendo hicho. …….………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… e) Yakinisha sentensi hii. (alama 1) Hapa napo sipo ninapotaka ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… f) Changanua kwa vielelezo vya mistari / vishale. (alama 3) Mwanafunzi anapohepa shuleni huadhibiwa kikondoo. g) Andika kwa udogo (alama 2) Mtoto wa mzee yule aligongwa kwa nyundo alipofukuzwa na mbwa. ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… h) Tumia kiunganishi alakulihali katika sentensi ili kubainisha matumizi yake. (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… i) Akifisha sentensi hii mtafanya kazi hii mpaka lini mzee alisema nataka ikamilike leo kesho mtaanza nyingine ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… j) Tunga sentensi ukitumia ‘A’unganifu mwafaka pamoja na nomino ulizopewa (alama 2) (i) Teo ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Liwali ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… k) Eleza matumizi ya ni katika sentensi ifuatayo: (alama 2) Rudini haraka! Amina ni mgeni hapa kwetu, nitamtembeza mjini ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… l) Vitumie vihisishi vifuatavyo katika sentensi. (alama 2) (i) Ebo! ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Kefule! ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… m) Sentensi hizi zinaashiria nyakati gani? (alama 2) (i) Ninapokimbia huchoka sana ………………………………………………………………………………… (ii) Aendapo msikitini hujitia tohara ………………………………………………………………………………… n) (i) Imekuwa vigumu mwananchi kuelewa katiba (andika katika kauli ya kutendea) (alama 1) ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Andika sentensi katika kauli ya kutendewa ukitumia kitenzi ‘cha’ (alama 1) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… o) Tumia vivumishi vya pekee kutunga sentensi zenye maana ifuatayo. (alama 2) (i) bila kubagua ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) bila kubakisha ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… p) Eleza maana mbili za sentensi hii (alama 2) Alinichezea na Baniani ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… q) Tunga sentensi mbili tofauti kubainisha maana tofauti kati ya: (alama 2) (i) Pamba ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… (ii) Bamba ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… r) Mwalimu huyu atawatahini wanafunzi wote watakaofanya mtihani. (alama1) Anza: Wanafunzi wote ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………… s) Unda kitenzi kutokana na nomino hii (alama 1) Nomino kitenzi Ufisadi 1. MATUMIZI YA LUGHA a) (i)/w/,/y/ (2x1=2) (ii) /k/ /sh/ (2x½=1) b) Yambwa tendwa – josho Yambwa tendewa – wanakijiji (2x1=2) c) Nilimjibu (kuwa / kwamba) singeenda sokoni siku hiyo ila ningeenda siku iliyofuata (6x½=3) d) Wale – kiwakilishi kionyeshi / kiashiria Wale – kivumishi kionyeshi / kiashiria Wale - kitenzi e) Hapo napo ndipo ninapotaka Hapo napo ndipo nitakapo (yoyote 1x1=1) f) S – KN +KT KN – N + S N – Mwanafunzi S – anapohepa shuleni KT – T + E T – huadhibiwa E - kikondoo (6x½=3) g) Kitoto cha kizee kile kiligongwa kwa kijundo kilipofukuzwa na kijibwa. (8x¼=2) h) Alakulihali – kwa vyovyote vile. i) “Mtafanya kazi hii mpaka lini? “Mzee alisema, “Nataka ikamilike leo, kesho mtaanza nyingine.” (kutuza) 1- 0 2-½ 3-1 4-1 ½ 5-2 6- 2½ 7- 3 8- 3½ 9- 4 j) Teo za Abunuasi zimepotea Liwali wa kwanza amewasili shambani (2x1=2) k) Rudini -wingi wa wahusika ni -kitenzi kishirikishi kipungufu. nitamtembeza – kiambishi kiwakilishi cha nafasi (kiambato/tegemezi) mjini - kielezi l) (i) Ebo! Kuonyesha dharau (ii) kefule! Kinyume na matarajio (hasa kuhusu maadili) (2x1=2) m) (i) wakati maalumu (ii) Wakati wowote (2x1=2) n) (i) Imewia wananch vigumu kuelewa katiba (1x1=1) (ii)cha – chiwa (1x1=1) o) (i)-o-ote (ii)-ote (2x1=2) p) Mimi pamoja na Baniani tulichezewa. Yeye pamoja na Baniani walichezewa (2x1=2) q) (i) Pamba (i) sufi ya mmea iliyo nyeupe na laini (ii) chakula au masurufu ya wakati wa safari (iii) visha mavazi mazuri ya kupendeza (iv) tia urembo (v) tayarisha au panga vitu kwa uzuri (vi) kuwa mahali aghalabu watu au wadudu (ii)bamba (i) kamata mtu kwa nguvu”baka” (ii)ziba au zuia (iii)bati (iv) kitu chembamba chenye ubapa (bamba la upanga) r) Wanafunzi wote watakaofanya mtihani watatahiniwa na mwalimu huyu. (1x1=1) s) Ufisadi fisidi (1x1=1)
0 Comments
Leave a Reply. |
Categories
All
Archives
July 2024
|
We Would Love to Have You Visit Soon! |
Hours24 HR Service
|
Telephone0728 450425
|
|
8-4-4 materialsLevels
Subjects
|
cbc materialsE.C.D.E
Lower Primary
Upper Primary
Lower Secondary
Upper Secondary
|
teacher support
Other Blogs
|