Maswali na Majibu KCSE Kiswahili
Ufahamu | Ufupisho | Isimu Jamii | Insha | Utumizi wa Lugha
SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (Alama40) a) Tofautisha sauti zifuatazo. (alama 2) /a/ /u/ __________________________________________________________________________ b) i) Ngeli ni nini? (alama 1) __________________________________________________________________________ ii) Maneno haya yamo katika ngeli gani? (alama 2) Tayo __________________________________________________________________________ Kipepeo __________________________________________________________________________ c) Akifisha sentensi hii kwa njia tatu tofauti kuleta dhana tatu tofauti. (alama 3) Babu alimchapa nyanya __________________________________________________________________________ d) Ainisha mofimu katika neno lifuatalo (alama 3) Sikumkaribisha __________________________________________________________________________ e) Andika katika usemi wa taarifa (alama 3) “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim __________________________________________________________________________ f) Andika kwa wastani (alama 2) Magoma hayo yatachezwa mawanjani __________________________________________________________________________ g) Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani h) Tofautisha sentensi zifuatazo. (alama 2) i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri ii) Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri __________________________________________________________________________ i) Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya: (alama 3) a) Kulinganisha __________________________________________________________________________ b) Sababu __________________________________________________________________________ c) Wakati __________________________________________________________________________ j) Kwa kutoa mifano katika sentensi onyesha matumizi mawili ya parandesi (alama 2) __________________________________________________________________________ k) Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo (alama 4) Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana. __________________________________________________________________________ l) Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi (alama 2) i) Nisimamapo huchekwa ii) Ninaposimama huchekwa __________________________________________________________________________ m) Andika sentensi hii upya bila kubadilisha maana ukitumia ‘o’ rejeshi na kiambishi ngeli mwanafunzi alitumwa nyumbani juzi na hajapata karo hadi leo. __________________________________________________________________________ n) i) Eleza dhana ya kishazi tegemezi (alama1) __________________________________________________________________________ ii) Bainisha aina za vishazi (alama 2) Konde iliyopaliliwa ilituletea mazao mengi sana __________________________________________________________________________ o) Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma (alama 2) __________________________________________________________________________ Mwongozo
a) /a/ ni irabu ya kati (hutamkwa kwa kutumia sehemu ya kati ya ulimi) midomo hutandanzwa inapotamkwa. /u/ ni irabu ya nyuma (ulimi huinuliwa juu na kupindwa nyuma ya inapotamkwa. midomo kuviringwa inapotamkwa. b) i) Ngeli ni kundi la nomino za aina moja ii) Tayo – LI – YA Kipepeo – A – WA c) Babu alimchapa nyanya? (swali) Babu alimchapa nyanya! (mshangao) Babu alimchapa nyanya. (maelezo / taarifa) d) si – kiwakilishi cha ukanushaji ku – kiwakilishi cha wakati uliopita m – kiwakilisha cha mtendwa karib – mzizi ish – kiwakilishi cha kauli a – kiishio e) Salim alisema kwamba wangepata mwaliko wao siku iliyofuata au Salim alisema kuwa tungepata mwaliko wetu siku iliyofuata. f) Ngoma hizo zitachezwa uwanjani g) S – KN + KT KN – N + V + N N - Wanafunzi V – wenye N – bidii KT – T + N T – hufuzu N – mtihani h) i) Nge – huonyesha wakati ujao na kuwa kuna uwezekano ii) Ngali – huonyesha wakati uliopita na hakuna uwezekano / ni majuto i) a) Abunuwasi ni mjanja kama sungura Dhahabu ni ghali kuliko shaba b) Juma ametuzwa kwa uhodari wake c) Jogoo huwika kabla ya saa tisa usiku j) Jona (kijana mpole) anasafiri leo kwenda mjini? maelezo ya ziada Aziza (mhusika mkuu) aliomba talaka Mjomba: (akikohoa) habari? – tamthilia / mazungumzo Kufungia nambari (1) (2) (3) k) Nyanya – kiima Mjukuu – shamirisho kitondo Nyumba – shamirisho kipozi Chagizo – i) mwaka jana ii) kwa matofali Shamirisho ala – matofali Alimjengea – kiarifa l) i) Wakati wowote ii) Wakati maalumu m) Mwanafunzi aliyetumwa nyumbani juzi, hajapata karo hadi leo. n) Kishazi tegemezi – ni kundi la maneno lililo na kiima na kiarifa lakini haliwezi kujisimamia pekee kama sentensi. hutegemea kishazi huru ili kupata maana. o) Watoto hao wanachuma machungwa Nondo za madirisha hutengenezwa kwa chuma Mimi ninafanya kazi ili kuchuma pesa
0 Comments
Leave a Reply. |
Categories
All
Archives
June 2024
|
We Would Love to Have You Visit Soon! |
Hours24 HR Service
|
Telephone0728 450425
|
|
8-4-4 materialsLevels
Subjects
|
cbc materialsE.C.D.E
Lower Primary
Upper Primary
Lower Secondary
Upper Secondary
|
teacher support
Other Blogs
|